KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 24, 2016

KUZIONA YANGA, AZAM BUKU TANO



KIINGILIO cha chini katika Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kati ya Yanga SC na Azam FC kitakuwa ni Sh.5,000.
 

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema leo kwamba kiingilio cha Sh. 5,000 kitahuus majukwaa yote ya mzunguko. Lucas ametaja viingilio vingine kuwa ni Sh 25,000 kwa VIP A na Sh 20,000 kwa VIP B na C.

Sherehe za mchezo huo zitaanza rasmi saa 8.00 mchana kwa mchezo wa awali wa kuburudisha kuzikutanisha timu za soka za kituo cha Televisheni cha Azam ‘Azam Tv’ na wafanyakazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kurushwa live na kituo hicho kilichotokea watazamaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

No comments:

Post a Comment