KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, May 23, 2016

YANGA, AZAM SASA KUKIPIGA KESHO FAINALI YA KOMBE LA FA


Fainali za kuwania Kombe la Shirikisho, maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC), zitakazokutanisha timu za soka ya Young Africans na Azam FC, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa zitafanyika kesho (Mei 25, 2016) kama ilivyotangazwa awali.

Awali fainali hizo zilipangwa Juni 11, 2016 ili kuzipa muda wa kuajindaa timu mara baada ya michezo ya mwisho ya Ligi Kuu ya Vodacom inayotarajiwa kufikia ukomo Mei 22, 2016, lakini imeachwa tarehe ya awali ili kuenenda na kanuni ya tarehe ya mashindano kwani mwisho wa msimu ni Mei 31, mwaka huu.

Kadhalika tarehe ya awali ilipangwa kutokana ratiba kubana hasa ya timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ambayo ina mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Kenya ‘Harambee Stars’ unaotarajiwa kufanyika Mei 29, mwaka huu. Mchezo huo unaingia kwenye kalenda ya FIFA.

Taifa Stars itacheza mechi hiyo ikiwa ni maandalizi ya mchezo wake dhidi ya Misri unaotarajiwa kufanyika Juni 4, 2016 jijini Dar es Salaam kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).

Tayari TFF imefafanua iwapo Bingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu 2015/16 inayoendelea atashinda pia taji katika fainali za Kombe la Shirikisho la ASFC, ndiye atayeiwakilisha nchi katika michuano ya Ligi ya mabingwa wa Afrika msimu wa 2016/17.

Kwa msingi huo, timu itayopoteza fungwa katika fainali hizo za Kombe la Shirikisho –ASFC linalodhaminiwa na kituo cha Televisheni cha Azam, ndiyo itakayowakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika katika msimu wa 2016/17

Fainali za Kombe la Shirikisho zinakuja baada ya mchuano ulioshindanisha timu 64 za Ligi Kuu Tanzania Bara - VPL (16); Ligi Daraja la Kwanza -FDL (24), Ligi Daraja la Pili – SDL (24)

No comments:

Post a Comment