KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 26, 2016

YANGA BINGWA KOMBE LA FA


MABINGWA wa soka wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga jana walifanikiwa kuongeza taji lingine baada ya kuibwaga Azam mabao 3-1.

Yanga, ambayo imefuzu kucheza hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Afrika, imetwaa Kombe la FA, baada ya kuibuka na ushindi huo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Yanga imezawadiwa kitita cha sh. milioni 50, ikiwa ni siku chache baada ya kuzaliwa sh. milioni 80, kutokana na kutwaa ubingwa wa ligi kuu.

Mshambuliaji Amis Tambwe aliendelea kuibeba Yanga baada ya kuifungia mabao mawili kati ya matatu. Bao lingine lilifungwa na Deus Kaseke.

Bao la kufutia machozi la Azam lilifungwa na mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Didier Kavumbagu, aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya John Bocco.

No comments:

Post a Comment