KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, May 2, 2016

SIMBA, AZAM HAKUNA MBABE


MATUMAINI ya timu za Simba na Azam kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara, jana yaliingia doa baada ya kutoka suluhu katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Sare hiyo imezifanya Simba na Azam kuendelea kuwa nyuma ya Yanga, ambayo inaongoza kwa kuwa na pointi 65, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 59 na Simba yenye pointi 58.

Katika mchezo huo uliojaa ushindani wa kila aina, timu zote mbili zilicheza kwa kasi kwa lengo la kutafuta mabao, lakini umaliziaji mbovu ulikuwa kikwazo.

Mshambuliaji John Bocco ndiye aliyewanyong'onyeza mashabiki wa Azam baada ya kupoteza nafasi zaidi ya tatu nzuri za kufunga mabao, ambapo mashuti yake yalitoka nje ya lango.

No comments:

Post a Comment