KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 17, 2016

YANGA YAKIPASHA MOTO KIPORO CHA MTIBWA, YAICHAPA BAO 1-0 LIGI KUU


MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, Yanga jana walirejea kileleni mwa ligi hiyo baada ya kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga ilijipatia bao hilo la pekee dakika ya 59 kupitia kwa Simon Msuva.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 59 baada ya kucheza mechi 24, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 57 baada ya kucheza idadi hiyo ya mechi.

Hata hivyo, Simba inaweza kurejea tena kileleni mwa ligi hiyo leo iwapo itaifunga Toto African katika mechi nyingine ya ligi hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment