KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, December 4, 2015

MKUTANO MKUU WA TFF KUFANYIKA TANGA


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) linatarajia kufanya mkutano wake Mkuu wa Mwaka kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga ambapo wajumbe wa mkutano huo tayari walishatumiwa taarifa za mkutano.

Akiongea na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa mikutano wa TFF, Kaimu Mkurugenzi wa Sheria na Wachama, Elliud Mvela amesema maandalizi ya mkutano huo yanaendelea vizuri.

Mvella amesema ajenda za mkutano mkuu wa kawaida ni zile zilizopo kikatiba, ila itaongezeka ajenda ya marekebisho ya katiba ambayo ni mapendekezo yaliyotolewa na FIFA.

Agenda za mkutano mkuu ni:

1.Kufungua Mkutano

2. Uhakiki wa Wajumbe

3. Kuthibitisha Ajenda.

4. Kuthibitisha Muhtsari wa Mkutano Mkuu uliopita.

5. Yatokanayo na Mkutano uliopita.

6. Hotuba ya Rais.

7. Ripoti kutoka kwa Wanachama

8. Kuthibitisha ripoti ya utekelezaji wa Kamati ya Utendaji.

 9. Kuthibitisha ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu 2013.

10. Kupitisha bajeti ya 2016

11. Marekebisho ya Katiba

12. Mengineyo

13. Kufunga Mkutano.

No comments:

Post a Comment