KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, December 4, 2015

MKUTANO MKUU TPLB DESEMBA 13


Mkutano Mkuu wa Pili wa Kawaida wa Baraza Kuu (Ordinary Governing Council) la Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) utafanyika Jumapili, Desemba 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Mkutano wa Kawaida ambao wajumbe wake ni klabu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza utafanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Uwanja wa Taifa kuanzia saa 4 kamili asubuhi.

Ajenda za Mkutano huo ni Kufungua mkutano, Kuhakiki akidi, Kuthibitisha ajenda, Kuthibitisha Muhtasari wa Mkutano uliopita, Yatokanayo na Mkutano uliopita, Hotuba ya Mwenyekiti, Kupokea Taarifa za Utekelezaji kutoka kwa Wanachama, Kuthibitisha Taarifa ya Utekelezaji ya Kamati ya Uongozi, Kuthibitisha Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu, na Kupitisha Bajeti ya 2016.

Mkutano huo utakuwa chini ya Mwenyekiti wake Hamad Yahya Juma

No comments:

Post a Comment