KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, December 19, 2015

SIMBA YABANWA MBAVU NA TOTO AFRICAN SPORTS


SIMBA leo imeshindwa kuonyesha makucha yake mbele y Toto African ya jijini Mwanza baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Simba ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 22 kupitia kwa mshambuliaji wao Danny Lyanga huku Toto ikisawazisha dakika za nyongeza mfungaji akiwa ni Evarist Bernard ambaye aliingia kuchukuwa nafasi ya Miraji Athuman dakika ya 71.

Hiyo ni sare ya pili mfululizo kwa kikosi cha Simba baada ya kulazimishwa sare kwenye mchezo wao uliopita dhidi ya Azam wakienda sare kwa kufungana bao 2-2 uwanja wa taifa.

Katika Uwanja wa Mwadui Complex, wenyeji Mwadui wameifunga Ndanda FC mabao 2-1, mabao ya Mwadui yalifungwa na Jerry Tegete na Jabir Azizi wakati bao la Ndanda lilifungwa na Atupelek Green huku Kagera Sugar ikiifunga African Sports bao 1-0, bao lililofungwa kwa penalti na Salum Kanoni.

Azam wao wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 26 na wamecheza mechi 10 ambapo kesho watacheza na Majimaji kwenye Uwanja wa Majimaji uliopo Songea.

No comments:

Post a Comment