KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, December 26, 2015

YANGA YACHANJA MBUGA, SIMBA YASONONESHA MASHABIKI WAKE


YANGA SC imetanua mbawa kileleni mwa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo unaifanya Yanga SC ifikishe pointi 33, baada ya kucheza mechi 13, wakati Azam FC iliyocheza mechi 12, ina pointi 29.
Mrundi Amissi Tambwe aliifungia Yanga SC mabao mawili mfululizo, la kwanza dakika la 37 akimalizia pasi ya winga Simon Msuva na la pili dakika ya 65 akimalizia krosi ya Mwinyi Hajji Mngwali, kabla ya kumpasia kwa kichwa Mzimbabwe Thabani Kamusoko kufunga la tatu dakika ya
66.
katika mchezo mwingine wa ligi hiyo, Simba SC imelazimishwa sare ya 1-1 na Mwadui FC ya kocha Jamhuri KIhwelo ‘Julio ’Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.


Mwadui walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Nizar Khalfan dakika ya 77, kabla ya Brian Majwega kuisawazishia Simba SC dakika ya 86.

CHANZO CHA HABARI: BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment