KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 7, 2015

KOMBE LA SHIRIKISHO KUENDELEA DESEMBA 15

Michezo ya Kombe la Shirikisho nchini (Azam Sports Federation Cup) mzunguko wa pili unatarajiwa kuendelea kuanzia Disemba 15 mwaka huu, ambapo jumla ya timu 32 zitachuana kusaka nafasi ya kuingia mzunguko wa tatu wa kombe hilo.

Mzunguko wa kwanza uliochezwa mwezi Novemba, jumla ya timu 32 zilichuana kutoka Ligi Daraja la Pili, na timu 16 kusonga mbele hatua ya pili inayozikutanisha timu za Ligi Daraja la Kwanza (StarTimes League) 16 na kufanya idadi ya timu 32 zinazosaka kufuzu kwa hatua ya mzunguko wa tatu.

Timu zilizofuzu kwa mzunguko wa pili kutoka mzunguko wa awali ni Abajalo FC, Mshikamano FC, Green Warriors, Villa Squad (Dar), Mvuvuma FC (Kigoma), Madini FC (Arusha), Sabasaba FC (Morogoro), Alliance, Pamba FC (Mwanza), Mighty Elephant (Songea), Kariakoo FC (Lindi), Wenda (Mbeya), Singida United (Singida).

Timu za Daraja la Kwanza zinaoanza kucheza mzunguko wa pili ni Polisi Tabora, Rhino Rangers, Burkinafaso, Friends Rangers, KMC, African Lyon, Ashanti United, JKT Oljoro, Panone FC, Kiluvya United, Lipuli FC, Kurugenzi, Mbao FC, Geita Gold, JKT Mlale, Njombe Mji, Kimondo, Mji Mkuu na JKT Kanembwa.









No comments:

Post a Comment