KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 22, 2015

AZAM YAIBANJUA NDANDA 1-0


BAO pekee la beki Shomary Salum Kapombe limeipa ushindi wa bao 1-0 Azam FC dhidi ya wenyeji, Ndanda FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Nangwanda, Sijaona, Mtwara.
Kapombe alifunga bao hilo dakika ya 79 kwa kichwa akimalizia krosi ya mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche.
Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ifikishe poniti 19, sawa na mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga SC wanaoendeleza kuongoza ligi hiyo kwa wastani wa mabao.
Kikosi cha Azam FC leo kilikuwa; Mwadini Ali, Shomary Kapombe, Gadiel Michael, Aggrey Morris, Serge Wawa Pascal, Said Mourad, Frank Domayo, Himid Mao, Ame Ali ‘Zungu’/Khamis Mcha, Kipre Tchetche/Jean Mugiraneza na Ramadhani Singano ‘Messi’/John Bocco.
Mechi nyingine za ligi hiyo leo, Mwadui FC wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Mgambo JKT Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.
Mabao ya Mwadui leo yamefungwa na Jerry Tegete dakika ya saba na 32 na Jamal Mnyate dakika ya 75, wakati bao pekee la Mgambo limefungwa na Abuu Daudi dakika ya 64.
JKT Ruvu imetoka sare ya 0-0 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Karume, Dar es Salaam wakati Mbeya City imeshinda 1-0 dhidi ya African Sports ya Tanga bao pekee la Geoffrey Mlawa dakika ya 15 Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

No comments:

Post a Comment