KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 20, 2015

SDL KUENDELEA NOVEMBA 14



Ligi Daraja la kwanza nchini (SDL) sasa itaanza Novemba 14 badala ya Oktoba 31 ili kutoa fursa kwa bodi ya Ligi kukamilisha maandalizi mengine ikiwemo viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michezo ya ligi hiyo.

Makundi ya SDL ni kama ifuatavyo; Kundi A ni Abajalo FC (Tabora), Singida United (Singida), Mvuvuma FC (Kigoma), Milambo FC (Tabora), Green Warriors (Dar es Salaam) na Transit Camp (Dar es Salaam) wakati kundi B ni Bulyanhulu FC (Shinyanga), JKT Rwamkoma (Mara), Pamba FC (Mwanza), AFC Arusha, Madini FC (Arusha) na Alliance Schools (Mwanza).

Kundi C ni Kariakoo (Lindi), Mshikamano FC (Dar es Salaam), Cosmopolitan (Dar es Salaam), Abajalo FC (Dar es Salaam), Changanyikeni Rangers (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam). Kundi D ni African Wanderers (Iringa), Mkamba Rangers (Morogoro), Town Small Boys (Ruvuma), Wenda FC (Mbeya), Coca-Cola Kwanza FC (Mbeya) na Sabasaba United (Morogoro).

No comments:

Post a Comment