KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, June 15, 2015

TAIFA STARS YAFUNGWA 3-0 NA MISRI

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, leo imepoteza mchezo wake wa kwanza kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON mwaka 2017 baada ya kufungwa kwa mabao 3 - 0 na wenyeji Misri.

Taifa Stars ilicheza vizuri kipindi cha kwanza na hasa sehemu ya ulinzi ilifanya kazi ya ziada kuokoa mashambulizi ya washambuliaji wa timu ya Misri, na kupelekea kwenda mapumziko -0 - 0.

Kipindi cha pili Misri walifanya mabadiliko yaliyowapelekea kupata mabao hayo 3 ndani ya dakika 10, kupitia kwa Ramy Rabia(60), Basem Morsy(64) na Mohamed Salah (69).

Stars ilifanya mabadiliko ya kuwaingiza Frank Domayo, Saimon Msuva na Salim Mbonde na kufanya shambulizi kadhaa langoni kwa Misri lakini mashambulzi hayo yaliokolewa na walinzi wa timu ya Misri.

Mara baada ya mchezo huo, Taifa Stars inaondoka leo Alexandria kuelekea Cairo ambapo itaondoka na shirika la ndege la Ethiopia saa 8 usiku na kufika jijini Dar es salaam jumanne saa 7 mchana.

Tanzania: Deogratias Munish, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Aggrey Morris/Salim Mbonde, Nadir Haroub, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto/Saimon Msuva, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata, Amri Kiemba/Frank Domayo.

Misri: Ahmed El Shenawy, Ahmed Hegazy, Ramy Rabea, Mohamed Abd Elshafy, Hazem Emam, Mohamed Elneny, Ibrahim Salah, Mahmoud Abd Elmonem/Ramadan Soffiy, Mohamed Salah/Mostafa Ftahy, Doly Elgabay/Basem Morsy, Ahmed Hassan Meky.

DRFA YASIKITISHWA NA MATOKEO MABAYA YA TAIFA STARS.

Chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam DRFA,kimesikitishwa na
matokeo mabaya iliyoyapata timu ya taifa (Taifa Stars) kwa kufungwa mabao
3-0 dhidi ya Mafarao wa Misri,katika mchezo wake wa kwanza uliopigwa jana usiku ugenini wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika (AFCON).

Mwenyekiti wachama hicho,Almas Kasongo, amesema matokeo hayo
yamewafadhaisha mno watanzania wenye uchu wa kuona timu hiyo inapata matokeo mazuri yaliyokosekana kwa kipindi kirefu.

Amesema anaamini kuwa kikosi hicho kina wachezaji wazuri na wenye uwezo
lakini wamekuwa wakikosa mbinu za kufanya vizuri kwenye timu ya taifa hasa kwenye safu ya ushambuliaji,ikilinganishwa na uwezo wanaouonesha kwenye michuano ya ligi wakiwa na klabuzao.

Hata hivyo Kasongo amesema licha ya Stars kuanza vibaya katika harakati zake za
kuwania tiketi yamichuano hiyo ya afrika,bado nafasi ipo ya kujipanga upya
kwa kuanza kuangalia uwezo wa benchi la ufundi.

Aidha amesema DRFA inaamini kuwa Tff  inauwezo wa kutafuta mwarobaini wa
kutibu tatizo la matokeo mabaya kwa Starz,bila kumuonea mtu aibu.

No comments:

Post a Comment