KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 21, 2015

NOOIJ ATIMULIWA TAIFA STARS



KAMATI YA UTENDAJI YASITISHA AJIRA YA NOOIJ

Kamati ya utendaji ya Shirikishi la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Katika kikao chake cha leo pamoja na mambo mengine ilipitia mwenendo wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mchezo kati ya Tanzania na Uganda, kama sehemu ya tathmin ya mwenendo wa timu.

Kamati ya utendaji kwa kauli moja imeamua yafuatayo:

1.Ajira ya Kocha Mkuu Maart Nooij inasitishwa mara moja kuanzia  tarehe 21/June/2015.

2.Benchi lote la ufundi la Taifa stars limevunjwa kuanzia tarehe 21/06/2015.

3.Uongozi wa TFF utatangaza punde benchi jipya la ufundi la timu ya Taifa.

Wakati huo huo, timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars jana ilipigwa mweleka wa mabao 3-0 na Uganda katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani AFCON.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, Taifa Stars ilicheza chini ya kiwango, hali iliyowafedhehesha mashabiki wachache waliofika uwanjani kushuhudia mechi hiyo na kuamua kuwazomea wachezaji.

Kamati ya Utendaji ya TFF ililazimika kufanya kikao cha dharula baada ya Stars kufungwa mabao 3-0 na Uganda na kufikia uamuzi wa kumtimua Nooij.

Hata hivyo, baada ya mchezo huo, Nooij alisema hawezi kuondoka kwa matokeo ya uwanjani, kwa sababu ana mkataba hadi mwaka 2016.

TFF italazimika kumlipa Nooij dola za Kimarekani zisizopungua 125, 000 (sh. milioni 250,000) kwa kumvunjia mkataba, ambao ni mishahara yake ya miezi 10, kwa sababu kwa mwezi alikuwa analipwa dola 12,500 (sh. milioni 25).

Mabao mawili ya mshambuliaji Erisa Sekisambu na lingine la Farouk Miya yanahitimisha historia ya kocha huyo Mholanzi Tanzania.

Kipigo hicho kiliwakosesha wachezaji wa Taifa Stars donge nono la sh. milioni 1 kila mmoja ahadi iliyotolewa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi juzi.

Mchezo huo ni tano mfululizo Taifa Stars kufungwa chini ya Nooij, aliyerithi mikoba ya Mdenmark Kim Poulsen, Aprili, mwaka jana na kwa ujumla timu hiyo imecheza mechi tisa bila ya ushindi chini ya Mholanzi huyo.

No comments:

Post a Comment