KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, June 2, 2015

15 WAJITOKEZA KUWANIA UONGOZI COASTAL UNION

KUELEKEA Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Coastal Union tayari maandalizi
yameanza kukamilika kwa asilimia kubwa ambapo jumla ya wagombea kumi
na tano wamejitokeza kuchukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za
uongozi.

Akizungumza leo ,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema
katika uchaguzi mkuu nafasi ambazo wagombea wamejitokeza ni Mwenyekiti
ambapo nafasi hiyo amejitokeza Dokta Ahmed Twaha akiwa hapa mpinzani.

Nafasi ya makamu Mwenyekiti wamejitokeza wagombea wawili ambao ni
Salim Amiri na Hussein Abdull Ally ambao watachuana ili kuweza
kupatikana mshindi ambayo atachukua nafasi hiyo.

Aidha amesema kuwa katika nafasi ya Kamati ya utendaji wamejitokeza
wagombea kumi na mbili ambao watachuana na kubaki wajumbe watano
watakaounda kamati ya utendaji.

Amewataja waliojitokeza kuwania nafasi hiyo ni Albert Clement
Peter,Omari Mwambasha,Waziri Mohamed,Mohamed Ally “Dondo”,Mohamed
Maulid Rajabu,Abubakari Ahmed Machai,Aggrey Ally Mbapu,Hassani Omari
Bwana.

Wengine ambao wamejitokeza kuwania nafasi hiyo kuwa ni Abdallah Zuberi
Ally “Unenge”,Hassani Ramadhani Muhsin,Albert Clement Peter,Hussein
Ally Mwinyi Hamis na Salim Abasi Perembo.

No comments:

Post a Comment