KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 11, 2015

STARS KUWAFUATA MISRI KESHO


Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premier Lager, kesho siku ya ijumaa jioni inatarajiwa kuondoka Addis Ababa Ethiopia kuelekea nchini Misri tayari kwa mchezo wa siku ya jumapili.

Stars ambayo imeweka kambi ya mazoezi takribani kwa wiki moja sasa jijini Addis Ababa leo imeendelea na raiba yake ya mazoezi katika uwanja wa Taifa, amabpo leo imefanya mazoezi yake asububuhi tu.

Kocha mkuu wa Taifa Stars Mart Nooij amesema, anashukuru maendeleo ya kambi ni mazuri timu yake inafanya mazoezi katika viwanja viwili vizuri vilivyopo Addis Ababa, uwanja wa Taifa na  uwanja wa Benki ya Biashara ya Ethiopia.

Nooij amesema amekuwa akiwafundisha wachezaji wake kucheza mpira wa kasi na pasi za haraka haraka, jambo ambalo wachezaji wameonyesha kufuata vizuri maelekezo yake na kusema wanamuelewa vizuri.

Akiongelea mchezo dhidi ya Misri siku ya jumapili, Nooij amesema timu inakwenda kupambana kusaka matokeo mazuri katika mchezo, nafahamu tunaenda cheza ugenini, nimewaelekeza vijana wangu wanaocheza nafasi ya ushambuliaji kutumia vizuri nafasi tutakazozipata katika mchezo huo.

Aidha, Kocha Nooij amesema katika mpira hakuna kinachoshindikana, kambi ya wiki moja Addis Ababa imewasaidia wachezaji kukaa pamoja na kushika maelekezo yake vizuri, hivyo anaamini timu yake itafanya vizuri katika mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON.

Katika kikosi cha wachezaji wa 22 waliopo kambini jijini Addis Ababa hakuna mchezaji majeruhi, wachezaji wote wako vizuri kiafya, kifikra na morali ni ya hali ya juu kuelekea kwenye mchezo huo dhidi ya Mapharao.

Taifa Stars inatarajia kuondoka kesho jioni ijumaa kuelekea nchini Misri kwa shirika la ndege la Ethiopia majira ya saa 5 usiku na kufika Cairo majira ya saa 8 usiku, kisha kuunganisha safari ya kuelekea jijini Alexandria ambapo timu mchezo huo utakapofanyika.

Mchezo kati ya Misri dhidi ya Tanzania utachezwa katika uwanja wa Borg El Arab kuanzia majira ya saa 1 jioni kwa saaa za huku, sawa na saa 2 kamili usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Waamuzi wa mchezo huo wanatokea nchini Ethiopia ambapo ni Bamlak Tessema Weyesa (mwamuzi wa kati), Kinfe Yilma (mwamuzi msaidizi wa kwanza), na Wolday Hailerague (mwamuzi msaidizi wa pili).

Wakati huo huo, kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, (Taifa Stars) kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro kimeendelea kujifua katika uwanja wa Benki ya Biashara ya Ethiopia eneo la CMC asubuhi na jioni katika uwanja wa Taifa wa Addis Ababa.

Stars ambayo imeweka kambi jijini Addis Ababa imekua ikijifua mara mbili kwa siku, kuhakikisha wachezaji wanakua vizuri kuelekea katika mchezo dhidi ya timu ya Taifa  Misri mwishoni mwa wiki hii jijini Alexandria.

Hali ya kambi kiujumla ni nzuri, wachezaji wote ni wazima, wakiwa wenye ari, na morali ya hali ya juu katika maandalizi ya mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON mwaka 2017.

Kocha mkuu wa Taifa Stars mholanzi, Mart Nooij amekuwa akiwafundisha vijana wake mbinu mbali mbali kuelekea kwenye mechi dhidi ya Misri,  kuanzia sehemu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji kuhakikisha wanakua fit katika mchezo unaowakabili.

Ikiwa ni siku ya nne tangu Taifa Stars kuanza mazoezi yake jijini Addis Ababa, kocha Nooij amesema anashukuru vijana wake wanamuelewa vizuri anachowaelekeza, sasa timu inacheza mpira wa kasi na pasi za haraka haraka, vijana wamechangamka na morali ni ya hali ya juu kambini kuelekea kwenye mchezo unaowakabili.

Hali ya nidhamu kambini ni ya hali ya juu, wachezaji waanatambua umuhimu wa mchezo huo, na kikubwa wameahidi kupambana kusaka matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Misri.

“Katika mpira hakuna kinachoshindikana, sie tumejiandaa vizuri, naamini tutakapofika Misri tutafanya vizuri na kuwapa furaha watanzania, kikubwa watuombee kwa mwenyezi mungu, tuwe wazima mpaka siku ya mchezo, naamini tutafanya vizuri” alisema Nadri.

Stars inatarajiwa kuelekea jijini Cairo siku ya ijumaa, kisha kuunganisha katika jiji la Alexandria tayari kwa mchezo dhidi ya Misri utakaochezwa katika uwanja wa Boeg El Arab siku ya jumapili Juni 14, 2015.

No comments:

Post a Comment