KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, December 16, 2014

SIMBA YAMNASA BEKI WA MTIBWA SUGAR

HASSAN Ramadhani (kulia) akimdhibiti mshambuliaji Mrisho Ngasa wa Yanga katika moja ya mechi za ligi kuu ya Tanzania Bara.

KLABU ya Simba imekamilisha dirisha dogo la usajili kwa kumsajili beki Hassan Ramadhani kutoka Mtibwa Sugar.
Usajili wa beki huyo unaifanya Simba iwe imesajili wachezaji wapya wanne katika usajili wa dirisha dogo. Wengine niDan Sserunkuma, Simon Ssenrukuma na Juuko Jurshid.
Makamu wa Rais wa simba, Godfrey Nyange 'Kaburu, amesema usajili wa Kessy umezingatia matakwa ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mzambia Patrick Phiri.
Kaburu alisema kwa sasa wanaamini kuwa kikosi chao kimekamilika katika kila idara na kwamba wanayo nafasi kubwa ya kushika nafasi mbili za kwanza katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.
Simba imewatema kiungo Pierre Kwizera na mshambuliaji Amis Tambwe, ambaye tayari amejiunga na klabu ya Yanga.


No comments:

Post a Comment