KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, December 16, 2014

YANGA YAMTUPIA VIRAGO MAXIMO



KLABU ya Yanga imemtupia virago Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mbrazil Marcio Maximo pamoja na mshambuliaji Emerson.
Uamuzi huo wa Yanga ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo, kilichofanyika jana chini ya uongozi wa Mwenyekiti, Yussuf Manji.
Habari za uhakika kutoka ndani ya klabu hiyo zimeeleza kuwa, nafasi ya Emerson imechukuliwa na mshambuliaji Amis Tambwe kutoka Simba.
Kutimuliwa kwa Maximo na Emerson kumekuja siku chache baada ya Yanga kuchapwa mabao 2-0 na Simba katika mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kutimuliwa kwa Emerson, ambaye alipokelewa kwa mbwembwe nyingi huku akitajwa kuwa kiungo mahiri mkabaji, kumeifanya Yanga isaliwe na wachezaji watano wa kigeni.
Mbali na Tambwe, wengine ni Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite, Andrey Countinho na Mliberia, Sherman.

No comments:

Post a Comment