KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, December 14, 2014

SSENKURUMA, JUUKO WAMWAGA WINO SIMBA



Simon Sserunkuma akitia saini fomu za usajili za Simba baada ya klabu hiyo kukatisha mikataba ya wachezaji wake wawili wa kimataifa, wote raia wa Burundi, mshambuliaji Hamis Tambwe na Kiungo Pierre Kwizera, ikiwa ni siku moja tangu Simba kuifunga Yanga kwenye mchezo wa nani mtani Jembe.

Beki Juuko Murushid, akitia saini mkataba wa kuichezea Simba. Juuko aliichezea Simba dhidi ya Yanga katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar-es-Salaam na kuonyesha uwezo mkubwa na kuisaidia Simba kupata ushindi wa mabao 2-0. Kwa usajili huo, Simba sasa inao wachezaji watano kutoka  Uganda. Wachezaji hao ni  George Owino, Emmanuel Okwi, Dan Sserunkuma, Saimon Sserunkuma na Juuko Murushid

No comments:

Post a Comment