KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 8, 2014

TAIFA STARS YA MABORESHO KUKIPIGA NA BURUNDI LEO


Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kimerejea Dar es Salaam kutoka Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambapo kiliweka kambi kwa ajili ya mechi ya kimataifa dhidi ya Burundi itakayochezwa leo.


Timu hiyo ambayo jana asubuhi ilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) juzi kwa ndege ya Fastjet saa 12.30 jioni na kwenda moja kwa moja kambini hoteli ya Tansoma.

Nayo timu ya Taifa ya Burundi ilitua nchini jana saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir. Kikosi hicho kitafikia hoteli ya Tiffany Diamond kitakwenda moja kwa moja Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo kitafanya mazoezi kuanzia saa 11 jioni.

Kiingilio cha mechi kati ya Tanzania na Burundi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni kitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya raungi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C ni sh. 5,000 tu.

No comments:

Post a Comment