KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 19, 2014

SIMBA, YANGA HAKUNA MBABE


 MSHAMBULIAJI Elias Maguri wa Simba akitafuta mbinu za kumtoka beki Oscar Joshua wa Yanga
 AMRI Kiemba wa Simba akiwania mpira na Andrey Coutinho wa Yanga
 KIPA Manyika Peter wa Simba akidaka mpira mbele ya washambuliaji wa Yanga
MSHAMBULIAJI Denilson Jana (namba 9) akikokota mpira huku akichungwa na kiungo Jonas Mkude wa Simba
TIMU kongwe za soka nchini, Simba na Yanga jana zilishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Sare hiyo ilikuwa ya nne mfululizo kwa Simba tangu ligi hiyo ilipoanza Septemba 29 mwaka huu na ya kwanza kwa Yanga, ambayo imeshinda mechi mbili, kupoteza moja na kutoka sare moja.

Katika mechi hiyo, kivutio kikubwa kilikuwa kipa chipukizi wa Simba, Manyika Peter, ambaye alilazimika kukaa langoni baada ya makipa Ivo Mapunda na Hussein Sharrifu kuwa wagonjwa.

Licha ya kuwa mechi yake ya kwanza katika ligi hiyo, timu ikizihusisha timu hizo kongwe, Manyika alionyesha umahiri mkubwa wa kulinda lango lake na kuwafanya mashabiki wa Simba wamshangilie kila alipodaka ama kuokoa mpira wa hatari.

Timu hizo zilicheza kwa kukamiana tangu mwanzo wa mchezo huku mabeki Nadir Haroub 'Cannavaro', Mbuyu Twite, Kevin Yondan na Oscar Joshua wakimwekea ulinzi mkali mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Simba.

Nao mabeki Joseph Owino, Hassan Isihaka, Lucian Gallas na Idrisa Rashid, waliwawekea ulinzi mkali Genilson Santos 'Jaja' na Andrey Coutinho, ambao walishindwa kufurukuta.

Timu zote mbili zilipata nafasi kadhaa nzuri za kufunga mabao, lakini zilipotezwa na washambuliaji wake, Jaja wa Yanga, Okwi na Elias Maguri wa Simba kutokana na mashuti yao kushindwa kulenga lango.

No comments:

Post a Comment