KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 8, 2014

BENIN YATAJA NYOTA WAKE WATAKAOIVAA STARS




Kocha wa timu ya Taifa ya Benin, Olle Didier Nicolle ametaja kikosi cha wachezaji 18 kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili (Oktoba 12 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mfaransa huyo ameita wachezaji 13 wanaocheza nje ya nchi hiyo akiwemo kiungo Stephane Sessegnon wa West Bromwich Albion ya Uingereza kwa ajili ya mechi hiyo ya Kalenda ya FIFA itakayoanza saa 11 jioni.

Wachezaji wengine katika kikosi hicho ni Didier Sossa (AS Dragons FC de I’Oueme, Benin), Abdel Fadel Suanon (Etoile Sportive du Sahel, Tunisia), Jodel Dossou (FC Liefering, Austria), Sessi D’almeida (FC Girondis Bordeaux, Ufaransa), Mohamed Aoudo (JS Saoura, Algeria) na Saturnin Allagbe (US Krake, Benin).

Steve Mounie (HSC Montpellier, Ufaransa), Farnolle Fabien (Clermont Foot Auvergne 63, Ufaransa), Jordan Adeoti (SM Caen, Ufaransa), Michael Pote (Omonia Nikosia, Cyprus), David Djigla (FC Girondis Bordeaux, Ufaransa) na Seidou Baraze (Kawkab Marrakech, Morocco).

Jean Ogouchi, Centre Mberie Sportif Club, Benin), Nafiou Badarou (ASO Chlef, Algeria), Eric Tossavi (Avrankou Omnisport, Benin), Fortune Ore (US Krake, Benin) na Seibou Mama (US Krake, Benin).

Msafara wa timu hiyo utaanza kuingia nchini kesho (Oktoba 9 mwaka huu) kwa nyakati tofauti, na utakuwa umekamilika (Oktoba 10 mwaka huu). Timu hiyo itafikia hoteli ya JB Belmont.

TFF YATIMIZA MIAKA 50 YA UANACHAMA FIFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo (Oktoba 8 mwaka huu) linaadhimisha miaka 50 ya kujiunga na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Katika kuadhimisha siku hii TFF ilipanga kufanya tafrija fupi ya kuwaenzi wale wote waliotoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya mpira wa miguu Tanzania katika kipindi hicho cha miaka 50.

Hafla hii itafanyika katika siku nyingine itakayopangwa. Orodha kamili ya watunukiwa imeambatanishwa hapa (attached).

No comments:

Post a Comment