KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 1, 2014

TAMASHA KUBWA LA FILAMU KUFANYIKA TANGA



MENEJA Masoko wa kinywaji cha Grand Malt Tanzania, Fimbo Buttala akizungumza na
waandishi wa habari katika ukumbi wa Kebbys Hotel juu ya uzinduzi wa Tamasha la
Filamu jijini Tanga litakalofanyika kuanzaia Jumamosi hadi Oktoba 8, mwaka huu.

TAMASHA la wazi la filamu Tanzania “Grand Malt Film Festival 2014” sasa litafanyika kuanzia Oktoba 4hadi 8 mwaka huu kwenye viwanja vya Tangamano jijinia Tanga imeelezwa.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Fimbo Butallah, alisema kuwa maandalizi ya tamasha hili yamekamilisha na uzinduzi rasmi utafanyika Jumamosi
Oktoba 4 na mgeni rasmi ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Halima Dendegu.

Butallah alisema kuwa tamasha hilo ni la wazi na hakuna kiingilio kwa wadau wa Sanaa hiyo ya filamu na uzinduzi utafanyika kuanzia saa tisa mchana.

Alisema kuwa kabla ya uzinduzi wa tamasha hilo, wasanii mbalimbali nyota ambao wanatarajia kushirikishi tamasha hilo watafanya kazi ya jamii kwa kutembelea kituo cha watoto wenye matatizo ya ngozi.

Aliongeza kuwa kupitia tamasha hili Grand Malt inasaidia kuinua na kutangaza kazi za wasanii wa hapa nchini na kuwapa nafasi ya kuwakutanisha na wadau na mashabiki wao.
Naye Kaimu Mwenyekiti wa Bongo Movie, Single Mtambalike, aliishukuru Grand Malt, kwa kufanikisha tamasha hili kwa mwaka wa tatu mfululizo.
Mtambalike alisema kuwa Sanaa ya filamu inasaidia kuwapatia ajira watu mbalimbali hapa nchini na kutaja katika maandalizi ya filamu moja, Zaidi ya wasanii 50 wanatumika kucheza filamu hiyo.

“Tunaashukuru sana Grand Malt na Sophia Records kwa kufanikisha tamasha hili ambalo linathibitisha wazi kuwa tasnia hii ni biashara kubwa”, alisema Mtambalike.

Rose Ndauka, ambaye naye ni msanii ya filamu aliwataka wadau wote kujitokeza na kutaja moja ya vitu watakavyotoa kwa watoto watakaowatembelea ni magodoro 60.

Awali tamasha hilo lilipangwa kufanyika mapema mwezi Agosti mwaka huu mkoani Mtwara.

No comments:

Post a Comment