KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 14, 2014

YANGA YAIENDEA SIMBA KAMBINI KUNDUCHI



Kikosi cha Young Africans Sports Club

Kuelekea kwenye mpambano wa watani wa jadi YANGA Vs SIMBA siku ya jumamosi Oktoba 18, kikosi cha timu ya Young Africans kimeingia kambini leo mchana katika hoteli ya Landmark iliyopo eneo la Kunduchi kujiandaa na mchezo huo ambao umeteka hisia za wapenzi wa soka nchini Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Kocha mkuu Marcio Maximo ameingia kambini na kikosi cha wachezaji 28 kujiandaa na mchezo huo ambapo kikosi chake kitakua kikifanya mazoezi katika Uwanja wa Boko - Veterani kila siku kujweka fit kwa kuzisaka pointi tatu muhimu siku ya jumamosi.

Akiongelea kuhusu maandalizi ya mchezo huo, Maximo amesema anashukuru vijana wake wote wapo katika hali nzuri kiafya, kifikra na morali ni hali ya juu kuelekea kwenye Dar Derby siku hiyo jumamosi.

Natambua mechi za wapinzani wa jadi huwa hazitabiriki, ila sisi kama Yanga tunajiandaa kuhakikisha tunapata ushindi katika mchezo huo dhidi ya Simba SC siku ya jumamosi, makosa yaliyokuwa yakijitokeza katika michezo iliyopita tumeshayafanyia kazi" alisema Maximo.

Wachezaji saba waliokuwa kwenye kambi ya timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) wameungana na wachezaji wengine leo wakiwa fit kabisa na hakuna mchezaji majeruhi hali inayompelekea kuwa na kikosi kipana cha maandalizi.

Wachezaji waliongia kambini kujianda na mchezo huo wa jumamosi ni:

Walinda mlango: Juma Kaseja, Ally Mustafa "Barthez" na Deo Munish "Dida"

Walinzi: Juma Abdul, Salum Telela, Oscar Joshua, Amos Abel, Edward Charles, Rajab Zahir, Pato Ngonyani, Kelvin Yondani, na Nadir Haroub "Cannavaro"

Viungo: Mbuyu Twite, Said Juma "Makapu", Omega Seme, Hamis Thabit, Nizar Khalfani, Issa Ngao na Haruna Niyonzima.

Washambuliaji: Geilson Santos "Jaja", Andrey Coutinho, Said Bahanuzi, Hamis Kizza, Saimon Msuva, Mrisho Ngasa, Hussein Javu na Jerson Tegete.

No comments:

Post a Comment