KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 12, 2014

TAIFA STARS YAIUA BENIN 4-1



 BEKI Shomari Kapombe wa Taifa Stars akiondosha mpira kwenye lango lake wakati timu hiyo ilipomenyana na Benin kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juzi.
 MRISHO Ngasa wa Taifa Stars akimfunga tela beki wa Benin wakati wa pambano hilo
HIKI ndicho kikosi cha Taifa Stars kilichoiua Benin jana

TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jana iliwapa raha Watanzania baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 4-1 dhidi ya Benin.

Katika mechi hiyo ya kirafiki ya kimataifa ya soka iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Taifa Stars ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 4-1.

Ushindi huo ulikuwa wa kwanza mkubwa kwa Taifa Stars dhidi ya timu kutoka mataifa ya Afrika Magharibi. Mara ya mwisho Taifa Stars kupata ushindi wa aina hiyo ilikuwa mwaka juzi wakati Taifa Stars ilipoichapa Morocco mabao 3-1 katika michuano ya Afrika.

Iliwachukua Taifa Stars dakika 16 kuhesabu bao la kwanza lililofungwa kwa kichwa na beki Nadir Haroub 'Cannavaro', akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Erasto Nyoni kutoka pembeni kidogo ya uwanja.

Kiungo Amri Kiemba aliwainua vitini mashabiki dakika ya 4 baada ya kuifungia Taifa Stars bao la pili baada ya kupokea krosi kutoka kwa Shomari Kapombe na kuwazidi mbio mabeki wawili wa Benin kabla ya kuubetua mpira ukampita kipa Farnoue Fabien.

Bao la tatu la Taifa Stars lilipatikana dakika ya 49 kupitia kwa Thomas Ulimwengu, akiunganisha mpira wa krosi uliopigwa na Mrisho Ngasa kutoka pembeni ya uwanja.

Juma Luizio, aliyetokea benchi kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ngasa, aliihakikishia Taifa Stars ushindi dakika ya 71 baada ya kuifungia bao la nne, akiunganisha krosi ya Ulimwengu.

Benin ilipata bao la kujifariji dakika chache kabla ya mpira kumalizika kupitia kwa Didier Sossa baada ya mabeki wa Taifa Stars kuzembea kumkaba.

No comments:

Post a Comment