KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 3, 2016

YANGA YAWEKEWA NGUMU NA PRISONS, ZATOKA SARE 2-2



YANGA SC imezidi kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni ya leo kulazimishwa sare ya 2-2 na Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Matokeo hayo hayaiondoi kileleni Yanga SC ikifikisha pointi 40 baada ya kucheza mechi 17, mbele ya Azam FC na Simba SC wenye pointi 39 kila mmoja.
Lakini Azam FC wana viporo wawili, wakati Simba SC ndiyo wamecheza mechi 17 kama Yanga.
Yanga SC walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 35 kupitia kwa mshambuliaji wake Mrundi, Amissi Tambwe aliyefunga kichwa akimalizia krosi ya kiungo Mnyarwanda, Haruna Niyonzima
Prisons wakasawazisha bao hilo kupitia kwa Jeremiah Juma Mgunda aliyefunga kwa kichwa pia dakika ya 40 akimalizia krosi ya Mohammed Mkopi.
Mkopi akaifungia Prisons bao la pili dakika ya 62 kwa kichwa pia akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na kiungo wa zamani wa Yanga SC, Juma Seif ‘Kijiko’.
Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Simon Msuva aliyetokea benchi kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Deus Kaseke aliisawazishia Yanga kwa penalti dakika ya 84 baada ya beki Meshak Suleiman kuunawa mpira kwenye boksi.

CHANZO CHA HABARI: BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment