KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 15, 2016

SIMBA HIYOOOOOOOO


MABAO mawili ya mshambuliaji Mganda, Hamisi Friday Kiiza yametosha kuipa Simba SC ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Stand United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Kwa ushindi huo, Simba SC inapanda kileleni mwa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu, ikifikisha pointi 45, baada ya kucheza mechi 19, ikiwazidi kwa pointi mbili, mabingwa watetezi, Yanga SC ambao hata hivyo wana mchezo mmoja mkononi. 

Kiiza alifunga mabao yake katika dakika za 34 na 47, hivyo sasa anaongoza kwa kufunga Ligi Kuu akifikisha mabao 16 dhidi ya 14, ya mshambuliaji wa mahasimu, Yanga SC, Mrundi Amissi Tambwe.
Stand United ilipata bao lake la kufutia machozi dakika ya 90 kupitia kwa David Ossuman. Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, African Sports imeifunga 1-0 Mgambo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati kocha Mmalawi, Kinnah Phiri ameanza na ushindi wa 5-1 dhidi ya Toto Africans Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Mabao ya MCC yamefungwa na Raphael Alfa kwa penalti dakika ya tano, baada kiungo mshambuliaji wa Mbeya City Ditrim Nchimbi kuchezewa vibaya kwenye boksi, Ramadhani Chombo 'Redondo' dakika ya 35, Haruna Moshi 'Boban', dakika ya 41 na 43 na Meshack Samueli dakika ya 79, wakati bao pekee la Toto lilifungwa na Japhet Mkala dakika ya 78.
Ndanda FC imeifunga 1-0 Majimaji Uwanja wa Nangwanda Sijaona.

No comments:

Post a Comment