KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 15, 2016

TFF YASIKITISHWA KAZIMOTO KUMPIGA MWANAHABARI



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa ya kupigwa kwa mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Mwanaspoti nchini, Mwanahiba Richard na kiungo wa timu ya Simba SC Mwiny Kazimoto mjini Shinyanga.

Kufuatia kitendo hicho kilichotokea wakati wa mazoezi, TFF imesema tukio liliofanywa na mchezaji huyo ni kinyume na sheria, taratibu/kanuni zinazoendesha mpira wa miguu nchini, hivyo wanakilaani kitendo hicho kwa nguvu zote.

Kwa kuwa tukio lilitokea wakati wa mazoezi, mpaka sasa TFF bado haijapokea taarifa rasmi kuhusiana na suala hilo.

No comments:

Post a Comment