KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 15, 2016

TFF YATUMA RAMBIRAMBI KWA MWANAHABARI HAMISI DAMBAYA


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa familia ya mwandishi wa habari za michezo nchini Hamis Dambaya kufuatia kufiwa na mkewe, mwanae pamoja mama mkwe wake.

Katika salamu hizo, TFF imempa pole Dambaya kwa msibu huo mzito uliomfika na kusema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini, Shirikisho liko pamoja nao katika kipindi hichi kigumu cha maombelzo ya misiba hiyo.

Mkewe Hamis Dambaya, mwanane na mama mkwe wake wamefariki katika ajali ya bus la Simba Mtoto iliyotokea leo asubuhi katikati ya eneo na Muheza na Hale wakati wakiwa safarini kuelekea jijini Dar es salaam wakitokea mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment