KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, February 19, 2016

LIGI KUU BARA KUENDELEA KESHO, SIMBA DIMBANI NA YANGA


Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuendelea wikiendi hii mzunguko wa 20 kwa michezo nane kuchezwa katika viwanja mbalimbali huku Jumamosi michezo mitano ikichezwa kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu katika ligi hiyo.

Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Yanga SC v Simba SC watakua wakichuana kusaka uongozi wa Ligi hiyo katika mchezo namba 153, huku Mgambo Shooting wakiwakaribisha Tanzania Prisons katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Wagonga Nyundo wa jiji la Mbeya, Mbeya City watawakaribisha Azam FC katika uwanja wa Sokoine mjini humi, mjini Shinyanga chama la wana Stand United watawakaribisha JKT Ruvu katika uwanja wa Kambarage, huku Toto Africans wakicheza dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Jumapili Ndanda FC watakua wenyeji wa African Sports uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, Mwadui FC watakua wenyeji wa Coastal Union uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga, huku wana lizombe Majimaji FC wakicheza dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Majimaji mjini Songea

Ligi Daraja la Pili (SDL) inatarajiwa kuendelea wikiendi hii katika mzunguko wa lala salama (raundi ya 9), kwa timu zote 24 kushuka dimbani pointi 3 muhimu katika msimamo ili kuweza kupanda ligi daraja la kwanza msimu ujao.

Jumamosi Kundi A, Green Warriors v Transit Camp (Mabatini), Singida United v Abajaro Tabora (Namfua), Mvuvumwa FC v Mirambo (Lake Tanganyika).

Kundi B, Jumapili Pamba FC v Madini FC (CCM Kirumba), AFC ARUSHA v Bulyanhulu (Sheikh Amri Abeid), huku Jumatatu Alliance School v JKT Rwamkoma (CCM Kirumba).

Jumamosi Kundi C, Cosmopolitan FC v Abajaro Dar (Karume), Jumapili Mshikamano FC v Kariakoo FC (Mabatini), Villa Squad v Changanyikeni (Karume).

Kundi D, Jumamosi African Wanderes v Mkamba Rangers (Wambi Mafinga), Jumapili Wenda FC v Sabasaba FC (Sokoine) huku Jumatatu The Mighty Elephant v Mbeya Warriors (Majimaji)

No comments:

Post a Comment