KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 10, 2011

Dakore afunga ndoa na Akande


BAADA ya usiri wa muda mrefu, hatimaye mwigizaji Dakore Egbuson amefunga ndoa na rafiki yake wa karibu, Olumide Akande, ambaye ni mtoto wa mwanasiasa, Harry Akande.
Habari za uhakika kutoka kwa watu wa karibu na Dakore zimeeleza kuwa, wapenzi hao walifunga ndoa rasmi Januari 16 mwaka huu mjini Lagos.
Kwa mujibu wa habari hizo, sababu kubwa ya kuchelewa kufungwa kwa ndoa hiyo ni wazazi wa Akande kumwekea masharti mkwe wao, wakimtaka aachane na kazi ya uigizaji.
Kufuatia masharti hayo, Dakore alikubali kuachana na kazi hiyo ili kutimiza nadhiri yake ya kufunga ndoa na Akande na pia kupata baraka za wakwe zake.

No comments:

Post a Comment