KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 5, 2015

YANGA MBELE KWA MBELE


WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho, Yanga wamefuzu hatua ya 16 bora licha ya kuchapwa bao 1-0 na Platnum ya Zimbabwe katika mechi iliyochezwa mjini Bulawayo.

Yanga imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-2, kufuatia kushinda mechi ya awali wiki mbili zilizopita mjini Dar es Salaam kwa mabao 5-1.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa itakutana na mshindi wa mechi kati ya Etoile du Sahel ya Tunisia na Benfica ya Angola.

Platnum walilianza pambano hilo kwa kasi huku wakiwa na uchu mkubwa wa kushinda kwa idadi kubwa ya mabao ili waweze kusonga mbele. Platnum ilikuwa ikihitaji ushindi wa mabao 4-0 ili isonge mbele kwa faida ya bao la ugenini..

Bao pekee na la ushindi la Platnum lilifungwa na mshambuliaji wao hatari, Walter Musona dakika ya 29 kwa shuti la mguu wa kushoto, akiunganisha krosi kutoka pembeni ya uwanja.

Yanga ilitarajiwa kurejea nchini juzi usiku kwa ndege ya serikali, ambayo ndiyo iliyowapeleka Zimbabwe.

No comments:

Post a Comment