KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 21, 2014

SIMBA YABANWA MBAVU NA COASTAL UNION



TIMU kongwe ya soka ya Simba jana ilitolewa jasho na Coastal Union baada ya kulazimishwa kutoka nayo sare ya mabao 2-2 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Simba itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka uwanjani na ushindi kwani ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 hadi mapumziko, yaliyofungwa na Shaaban Kisiga na Amisi Tambwe.

Uzembe wa mabeki wa Simba uliiruhusu Coastal Union kupata bao la kwanza dakika ya 68 lililofungwa na Yayo Lutimba kabla ya Ramadhan Salim kusawazisha dakika ya 81.

Kutokana na matokeo ya mechi za mwanzo za ligi hiyo, timu pekee iliyoibuka na ushindi mnono wa mabao ni Ndanda FC ya Mtwara, ambayo iliicharaza Stand United ya Shinyanga mabao 4-1.

No comments:

Post a Comment