KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, September 23, 2014

TASWA KUTETA NA WANAHABARI KESHO



Habari mdau, naomba kukujulisha kuwa kesho Jumatano Septemba 24, 2014, saa tano kamili asubuhi, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto, akiambatana na wadhamini washiriki wa Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania zinazoandaliwa na TASWA, watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kwenye mgahawa wa City Sports Lounge, Posta, Dar es Salaam kutangaza udhamini huo.


Pia katika mkutano huo, masuala ya Media Day Bonanza 2014 na mambo yahusiyo mafunzo kwa waandishi wa habari za michezo nayo yatazungumzwa.

Naomba ukipata taarifa hii, mjulishe na mwenzako. Karibu sana.

Ahsante,
Katibu Mkuu TASWA
0713-415346

No comments:

Post a Comment