KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, December 2, 2010

Z'bar yajiweka pabaya Kombe la Chalenji


TIMU ya soka ya Zanzibar, Zanzibar Heroes jana ilikwaa kisiki katika michuano ya Kombe la Chalenji baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Ivory Coast katika mechi ya kundi B iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kipigo hicho kimeiweka Zanzibar Heroes kwenye nafasi ngumu ya kutinga robo fainali, ambapo sasa italazimika kushinda mechi yake ya mwisho dhidi ya Rwanda itakayochezwa kesho.
Pamoja na kupata kipigo hicho, Zanzibar Heroes inashika nafasi ya pili katika msimamo wa kundi hilo, ikiwa na pointi tatu sawa na Ivory Coast, lakini ipo mbele kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Mshambuliaji Kipre Bolou ndiye aliyepeleka kilio kwa Zanzibar baada ya kuifungia Ivory Coast bao hilo pekee na la ushindi dakika ya 61. Alifunga bao hilo kwa shuti kali la umbali wa mita 30.
Katika pambano hilo, Ivory Coast ilionyesha kiwango cha juu cha soka, hasa kipindi cha kwanza kabla ya Zanzibar kushtuka dakika za mwisho, lakini washambuliaji wake walipoteza nafasi kadhaa za kufunga mabao.
Katika mechi nyingine ya kundi hilo iliyochezwa jana, Rwanda na Sudan zilishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu.
Pambano hilo halikuwa na msisimko mkali kutokana na timu zote mbili kushindwa kuonyesha soka ya kuvutia.

No comments:

Post a Comment