KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, November 25, 2014

KIIZA ATEMWA YANGA, NAFASI YAKE KUCHUKULIWA NA MZAMBIA


HATIMAYE Marcio Maximo, amekata mzizi wa fitina baada ya kumtema mshambuliaji wa kimataifa, Hamisi Kiiza katika kikosi hicho.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uganda ametemwa na nafasi yake inatarajiwa kujazwa na Mzambia Jonas Sakuwaha.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetangaza dirisha dogo la usajili kuwa Novemba 20 hadi Desemba 20, mwaka huu.

Maximo, alitarajia kuwasili jana usiku kutoka Brazil alikokwenda kwa mapumziko baada ya michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara kusimama kwa muda.

Habari za ndani kutoka Yanga zilidokeza kuwa kocha huyo amemuondoa, Kiiza, katika usajili wake kwa ajili ya kujiwinda na ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu.

Chanzo hicho cha uhakika kilisema, Sakuwaha, anatarajia kuwasili nchini wiki hii kufanya majaribio kabla ya kupewa mkataba endapo atamridhisha Maximo.

"Kocha ametoa maagizo kwa uongozi kumuengua (Hamisi) Kiiza na nafasi yake kujazwa na Mzambia wa TP Mazembe," alidokeza kigogo huyo.

Alisema ripoti ya Maximo ilitoa mapendekezo ya mchezaji huyo kutemwa kabla ya kuondoka nchini kwa mapumziko ya muda mfupi.

Sekuwaha, anatajwa kuwa mmoja wa washambuliaji hodari wa TP Mazembe, lakini Maximo, anataka kuona kipaji chake kwenye mazoezi kabla ya kumsajili.

Straika huyo anakuwa mchezaji wa pili wa kimataifa wa Yanga kuwania usajili katika dirisha dogo akiungana na Emerson De Oliveira Neves Rouqe kutoka Brazil.

Hivi karibuni Yanga ilisema Maximo anatarajia kuwasili nchini na siri nzito kuhusu mikakati yake ya usajili.

No comments:

Post a Comment