KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, November 25, 2014

KIEMBA: NIMEKUJA AZAM KUTAFUTA MAISHA




MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Simba, Amri Kiemba, amesema  kwenda kwake Azam ni kwa ajili ya kutafuta maisha yake kwani maisha popote sio sehemu moja.


Kiemba ameyasema hayo baada ya kusaini mkataba wa kuitumikia Azam na kudai kuwa ataitumikia kwa moyo mmoja timu hiyo.

Akizungumza na mwandishi wetu kiemba alisema, japokuwa ameichezea simba kwa muda mrefu lakini amepiti changamoto nyingi kama kuambiwa kiwango kimeshikaa mara mzee.

"Changamoto zipo lakini nimeyavumuila mengi ila kwa sasa nashukuru kwamba nimeenda sehemu salama na nitahakikisha kuwa nitaonyesha ujuzi wangu wote na kuitumikia vyema timu yangu mpya,"alisema

Alisema kuwa kila mtu yupo kwa ajili ya kutafuta maisha kwa hiyo ikitokea nafasi kama hiyo hainahaja kuicha ukizingatia kwamba azam pia ni timu bora na inawachezaji bora.

Kiemba alisema kuwa timu kubwa zinakuwa na changamoto nyingi mno hivyo uvumilivu na ujasiri ndio ulio mfikisha hapo alipo.

Aliwataka mashabiki wake wasiwe na wasiwasi na yeye kwani ataendelea na kasi yae ileile pia atakuzidisha ili kuhakikisha kila mechi anapangwa katika kikosi cha kwanza.

"Nitajitahidi kufanya mazoezi kwa bidii ili kuwahakikisha kuwa napata nafasi ya kwanza katika kikosi cha mwalimu,"alisema

No comments:

Post a Comment