KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 1, 2014

WANAMICHEZO BORA TASWA KUPEWA TUZO JUNI 27


Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kinatarajia kutoa tuzo za Wanamichezo Bora wa Tanzania wa mwaka 2013, Juni 27 mwaka huu.

TASWA inaomba radhi kutokana na kushindwa kufanya tuzo mwaka jana na hiyo ilitokana na sababu mbalimbali ikiwemo wadhamini kujitoa dakika za mwisho.

Kutokana na hali hiyo, TASWA kwa kushirikiana na Kamati Maalum ya Kusimamia Tuzo hizo imeanza tena mchakato wa kuwazawadia wanamichezo waliofanya vizuri kuanzia Januari 2013 hadi Aprili 2014.

Kamati imevipa jukumu vyama vya michezo mbalimbali kupendekeza majina ya wanamichezo wao waliofanya vizuri kwa kipindi hicho, isipokuwa kwa mpira wa miguu wa wanaume jukumu hilo limekabidhiwa kwa wahariri wa habari za michezo Tanzania.

Kutokana na hali hiyo, naomba upendekeze majina ya wanasoka bora watano wa Tanzania unaoona wanafaa kuwania tuzo hiyo kwa mwaka 2013/2014. Itapendeza ukitaja katika mapendekezo yako sababu zako kwa nini unafikiri anafaa kuwania tuzo hiyo.

Baada ya Kamati ya Tuzo kupitia majina yote, hatua itakayofuata itateua matatu yaliyopendekezwa sana na kuyarudisha kwa wahariri ili yapigiwe kura kuchagua mmoja.

No comments:

Post a Comment