KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 1, 2014

WAGOMBEA SITA WAENGULIWA UCHAGUZI WA SIMBA




KAMATI ya Uchaguzi ya klabu ya Simba, imewaengua wagombea sita kuwania nafasi walizoomba katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Juni 29 mwaka huu.

Wagombea walioenguliwa ni Selemani Dewji, Ahmed Mlanzi, Emmanuel Kazimoto, George Wakuganda, Omari Omari, Ramson Ritiginga na Salim Jaza waliokuwa wakiwania nafasi ya ujumbe.

Mbali na kuenguliwa kwa wagombea hao, wengine watano wamejitoa kutokana na sababu mbalimbali. Wagombea hao ni Asha Kigundula, Juma Pinto na Hussein Simba, waliokuwa wakiwania nafasi ya ujumbe.

Wengine ni Joseph Itang'are 'Kinesi' na Emmanuel Mayange waliokuwa wakiwania nafasi ya makamu wa rais.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Damas Ndumbaro, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, wagombea walioenguliwa ni kutokana na kutokidhi katiba ya Suimba ibara ya 26 (6).

Alisema wagombea hao wamekosa sifa, ambayo inaelezwa katika ibara hiyo, ambayo inamtaka mgombea kuwa mwanachama wa klabu hiyo kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.

Ndumbaro alisema wagombea wengine walikosa sifa, ambayo ipo katika ibara ya 26 (2), ya kuwa na elimu ya sekondari na wengine hawakuwa na vyeti hivyo.

Alisema wagombea waliojiengua walitoa sababu mbalimbali, ambazo kamati yake iliridhika nazo, zikiwemo za kifamilia.

Kwa mujibu wa Ndumbaro, licha ya mchujo uliofanywa na kamati yake, upo uwezekano mkubwa idadi ya wagombea kupungua baada ya uchunguzi unaofanywa na taasisi mbalimbali kwa baadhi ya wagombea kukamilika.

Alisema uchunguzi huo unafanywa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Wagombea waliopitishwa katika mchujo huo wa awali ni Andrew Tupa na Evans Aveva (rais). Wengine ni Bundala Kabulwa, Geofrey Nyange 'Kaburu', Jamhuri Kihwelo na Swedy Nkwabi (makamu wa rais).
Wajumbe ni Ally Suru, Abdulhamidi Mshangama, Alfred Lia, Ally Chaurembo, Amina Poyo, Asha Muhaji, Chano Karaha, Collin Frisch, Damian Manembe, Hamisi Mkoma, Ibrahim Masoud, Iddi Mkambala, Iddi Noor, Jasmin Badour, Juma Musa, Maulid Abdalla, Rodney Chiduo, Saidi Kubenea, Saidi Pamba, Daidi Tully na Yassin Mwete.

No comments:

Post a Comment