KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 23, 2015

YANGA YAICHAPA TELECOM 3 -0


Mabingwa mara tano wa michuano ya Kombe la Kagame timu ya Young Africans (Yanga SC) leo imeibuka na ushindi wa mabao 3- 0 dhidi ya timu ya Telecom kutoka nchini Djibout, katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Mabao ya Yanga yalifungwa na mshambuliaji Malimi Busungu aliyefunga mabao mawili, na Geofrey Mwashiuya  aliyefunga bao la tatu kwa kombora kali umbali wa mita 20 na kupeleka kilio kwa timu ya Telecom.

Katika mchezo wa leo Yanga walipoteza penati mbili zilizopigwa na washambuliaji wake Amissi Tambwe na Saimon Msuva zilizookolewa na mlinda mlango wa Telecom Nzokira Jeef.

Baada ya ushindi huo wa leo kocha mkuu wa Yanga, mholanzi Hans Van der Pluijm amesema vijana wake leo wamecheza vizuri na ndio manaa wameweza kuibuka na ushindi huo wa mabao 3- 0.

Aidha kocha huyo amesema kwa sasa wanajiandaa na mchezo wa siku ya ijumaa dhidi ya KMKM utakochezwa saa 10 kamili ijumaa, ukitanguliwa na mchezo kati ya Gor Mahia dhidi ya Khartoum utakoanza saa 8 kamili mchana.

Katika mchezo wa uliotangulia mapema saa 8 mchana, timu Khartoum ilibuka na ushindi wa mabao 2- 1 dhidi ya KMKM, huku katika uwanja wa Karume KCCA ya Uganda ikiibuka na ushindi wa bao 1-1 dhidi ya Adama City ya Ethiopia.

 KAGAME KUENDELEA LEO
Michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea kutimua vumbi jijini Dar es salaam itaendelea leo siku ya Alhamisi katika uwanja wa Taifa, ambapo Mabingwa mara tatu wa michuano hiyo timu ya APR SC watacheza dhidi ya LLB ya Burundi, mechi itakayoanza majira ya saa 10 kamili jioni.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha timu ya Heegan FC ya Somalia itakayocheza dhidi ya Al Shandy ya Sudan.

No comments:

Post a Comment