KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 22, 2015

MBEYA CITY YATANGAZA ZABUNI YA KUUZA VIFAA VYAKE VYA MICHEZO


TANGAZO LA ZABUNI LA UAGIZAJI NA UUZAJI WA VIFAA VYA CLUB.

Mbeya City Council F.C inakaribisha kampuni zenye uwezo wa kufanya kazi na
club yetu.

Kazi zinazotangazwa ni kama ifutazo:
I.      Kuwa mwagizaji wa vifaa mbalimbali vya club
II.     Kuuza vifaa mbalimbali vya club
Zabuni hii inafuati utekelezaji wa club kutaka kukuza mapato yake ili
iweze kujijenga msingi imala ya mapato na hivyo kuiwezesha kuendesha
shughuli zake mbalimbali.

Mwombaji anatakiwa atimize masharti yafuatayo.
1. Awe na Leseni hai ya biashara husika
2. Awe amesajiliwa kama mlipa kodi
3. Maelezo ya kampuni yaani Company profile ikieleza aina ya kampuni au
biashara unayoifanya na eneo ilipo.

4. Waombaji wawe ni makampuni yaliyosajiliwa kisheria na waambatanishe
vivuli vya nyaraka zinazoonyesha uhalali wa uwepo wa mwombaji. Pia
muombaji aonyeshe anwani ya ofisi yake (physical address).

5.Bahasha zenye zabuni zifungwe na lakiri zikionyesha jina na namba ya
zabuni inayoombwa zikielekezwa kwa anuni ya Katibu Mkuu Mbeya City Council
F.C, S.L.P 149, Mbeya na ziwasilishwe ofisi ya Timu iliyopo Ukumbi wa
Mkapa.
         Kwa maelezo wasiliana na;
         Katibu Mkuu
         Mbeya City  Council F.C
         S.L.P 149,Mbeya.
          Simu  N0: 0718732626

6.Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 03.08.2015 saa 4.00 asubuhi.

Katibu Mkuuu
Mbeya City Council F.C

No comments:

Post a Comment