KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 7, 2015

KOZI YA MAKOCHA WA MAGOLIKIPA JULAI 13


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF litaendesha kozi ya makocha wa magolikipa nchini itakayofanyika Julai 13 - 17, 2015 jijini Dar es salaam

Jumla ya makocha wa magolikipa 29 wanatarajiwa kuhudhuria kozi hiyo itakayofanyika katika ofisi za TFF zilizopo Karume.

Orodha ya Makocha watakaohudhuria kozi hiyo na timu wanazotokea kwenye mabano ni

Rafael Mpangala (Mgambo JKT), Adam Abdallah Moshi (Simba SC ), Khalid Adam Munnisson (Mwadui FC), Choke Abeid (Toto African), Mussa Mbaya (Ndanda FC), Idd Abubakar Mwinchumu (Azam FC), Herry Boimanda Mensady (Tanzania Prisons), Kalama Ben Lwanga (Stand United), Patrick Mwangata (Mtibwa Sugar), Juma Pondamali (Young Africans).

Wengine ni Abdi Said Mgude (Coastal Union), Razack Siwwa (African Sports Tanga), Josia Steven Kasasi (Mbeya City), Ramadhani Juma (Kagera Sugar Kagera),Abdallah Said Ngachimwa (JKT Ruvu), John Bosco (Majimaji FC Ruvuma), Fatuma Omary (Twiga Stars), Juma Kaseja Juma (Premier League), Athuman Mfaume Samata (Ilala), Peter Manyika John (Taifa Stars).

Hussein Tade Katadula (African Lyon), Juma Mohamed Bomba (Kinondoni), Mwameja Mohamed Mwameja (Ilala),  Agustino Malindi Mwanga (Kigoma), Mohamed Abbas Silima (Police SC. Zanzibar), Bakari Ali Kilambo (Kizimbani SC Zanzibar), Hafidh Muhidin Mcha (Zanzibar Heroes), Elyutery Deodatusy Mholery (Kinondoni), Salim Waziri (Tanga)



No comments:

Post a Comment