KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, November 17, 2011

Polisi Dom yawataka nyota saba wa Simba

KLABU ya Polisi Dodoma imeuandikia barua uongozi wa klabu ya Simba ikitaka kuwasajili wachezaji saba wa timu hiyo pamoja na aliyekuwa kocha msaidizi wa timu hiyo, Amri Said.
Wachezaji hao ni Shija Mkina, Amri Kiemba, Haruna Shamte, Salum Kanoni na wachezaji wa timu ya vijana wa chini ya miaka 20, Haruna Athumani na Edward Christopher.
Habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa, Polisi Dodoma imeomba kuwasajili wachezaji hao katika dirisha dogo la usajili linaloendelea hivi sasa.
Mtoa habari huyo alisema, uongozi wa Polisi Dodoma umevutiwa na viwango vya wachezaji hao na kusema iwapo watafanikiwa kuwasajili, wataiimarisha timu yao.
Kuhusu Amri Said, uongozi wa Polisi umesema wanamuhitaji kocha huyo ili kulisaidia benchi la ufundi la timu hiyo kwa kuwa ana uwezo mkubwa katika masuala ya uongozi.
"Tulimuona Amri Said wakati ule akiwa kocha msaidizi na uwezo wake tunaukubali na tunaamini kuwa, akija katika timu yetu, tutapata mafanikio,“ alisema.
Kufuatia barua hiyo, uongozi wa Simba umesema unatarajia kulifikisha ombi hilo kwa kamati ya Utendaji kabla ya kutoa ridhaa ya kuwaachia wachezaji hao.

1 comment: