KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 30, 2011

Masikini Mercy Johnson





LAGOS, Nigeria
NI vigumu kuamini, lakini habari za uhakika kutoka vyanzo mbalimbali ndivyo zinavyosema. Kwamba jicho la kulia la mwigizaji nyota wa filamu nchini Nigeria, Mercy Johnson limeharibika.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya habari, Mercy aliumia jicho lake hilo hivi karibuni wakati akiwa kwenye eneo la kuchezea filamu huko Asaba katika Jimbo la Delta.
Vyanzo hivyo vimesema mrembo huyo alipatwa na maumivu hayo baada ya kutokea ugomvi kati yake na mwigizaji mwenzake, ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Taarifa zinasema familia ya mcheza filamu huyo, aliyefunga ndoa hivi karibuni, imekuwa ikihaha ili kuhakikisha anafanyiwa operesheni ya kurekebisha jicho lake mjini London, Uingereza.
Kuumia kwa Mercy kumeelezwa kuwa, kumemtia majonzi makubwa kiasi cha kumfanya asiwe na raha huku akiwaza nini la kufanya ili aweze kurejea katika hali ya kawaida.
Gazeti la Sun la Nigeria lilijaribu kuwasiliana na Mercy mara kadhaa ili kupata ukweli wa tukio hilo, lakini simu yake imekuwa ikiita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
Filamu aliyokuwa akicheza Mercy imeandaliwa na Kampuni ya Magic Movies, imeandikwa na Micheal Jaja na kuongozwa na Jaja.

No comments:

Post a Comment