KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Hakuna kama Genevieve


LAGOS, Nigeria
KATIKA maisha yake ya usanii, Genevieve Nnaji ameshindwa kupata mafanikio katika fani moja pekee. Ni pale alipojaribu kujitosa kwenye muziki.
Hata hivyo, albamu ya Genevieve ilimpatia kiasi kikubwa cha pesa. Ni kwa sababu, mmiliki wa studio aliyorekodi albamu yake alimlipa fedha nzuri kwa ajili ya kazi hiyo.
Hiyo ni sehemu ndogo ya vikwazo, ambavyo mwanadada huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto amewahi kukumbana navyo.
Zaidi ya hapo, ni mtiririko wa matukio yenye mafanikio, si Nigeria pekee, bali katika bara zima la Afrika na sehemu zingine mbalimbali duniani.
Katika kipindi cha miaka sita iliyopita, hakuna mwigizaji filamu aliyeweza kupata mafanikio na kushinda tuzo nyingi kama Genevieve.
Msichana huyo, aliyekuwa akihisiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki D’Banj ameshinda tuzo zote alizoshiriki kuziwania na kuiwakilisha Nollywood sehemu mbalimbali duniani.
Genevieve pia amepata utajiri mkubwa kutokana na fani ya filamu na kuwa mwigizaji pekee wa kike anayelipwa fedha nyingi kwa kazi hiyo.
Hivi karibuni, Genevieve alikuwa miongoni mwa wacheza filamu nyota wa Nigeria waliopewa tuzo maalumu na Rais Goodluck Jonathan. Wengine walikuwa Olu Jacobs, Kanayo Kanayo, Amaka Igwe, Stephanie Okereke na Osita Iheme.
Mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Genevieve alisema ameamua kuitoa kwa mashabiki wake, ambao bila wao, asingeweza kupata mafanikio aliyonayo sasa.
“Tuzo hii ni kwa wale wote walioniunga mkono miaka yote hii na kusema ndio kwa kila jambo. Wapo waliosema hapana, lakini namshukuru Mungu,”alisema.

1 comment: