KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 16, 2011

Yvonne Nelson anusurika kufa


KUMASI, Ghana
MCHEZA filamu na mwanamitindo mwenye mvuto wa Ghana, Yvonne Nelson amenusurika kufa baada ya kula chakula chenye sumu.
Tukio hilo lilitokea Ijumaa iliyopita usiku, saa chache kabla ya Yvonne kupanda ndege kwenda Paris, Ufaransa.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa, Yvonne alikuwa akijiandaa kwenda Paris kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, akiwa na rafiki zake.
“Ilikuwa saa 6.30 usiku Ijumaa, alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata tiba. Alielezwa kwamba, alikula chakula chenye sumu,”kilisema chanzo hicho.
Akithibitisha tukio hilo, Yvonne alisema kupitia simu yake ya mkononi kwamba, anamshukuru Mungu kwa kuyanusuru maisha yake.
“Moja ya zawadi za kuzaliwa kwangu ilikuwa sindano. Mungu awajalie kila la heri,”alisema.
Kwa sasa, Yvonne yupo mjini Paris akishiriki katika kazi za miradi mbalimbali.
Mbali na kucheza filamu, Yvonne ni mmoja wa wanamitindo maarufu nchini Ghana, akishiriki kuonyesha mavazi ya wabunifu mbalimbali wa kimataifa.

1 comment: