KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Ati Ukwa ajigeuza demu!





LAGOS, Nigeria
MSANII machachari wa filamu za vichekesho nchini Nigeria, Osita Iheme hivi karibuni alitoa kali baada ya kuonekana hadharani akiwa amevaa kike.
Osita, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Ukwa, alitinga vivazi hivyo kwa nyakati mbili tofauti huku akiwa amesuka nywele zake.
Mbali na kusuka nywele zake kwa mtindo wa rasta, Ukwa pia alikuwa amepaka rangi ya mdomo na nyusi zake kuzikoleza rangi nyeusi. Alikuwa na mwonekano wa kike hasa.
“Osita amekuwa msichana!” Baadhi ya watu waliomwona walisikika wakisema.
Hali hiyo ilisababisha watu wengi iwapo Ukwa ameamua kufanya hivyo kwa makusudi ama alikuwa katika matayarisho ya kutengeneza filamu mpya.
Licha ya watu wengi kumshangaa, Ukwa alionekana kutojali huki akiendelea na mambo yake kama vile hakukuwa na jambo lililomshangaza.
Hata hivyo, baadhi ya watu waliohojiwa walisema wana hamu kubwa ya kuiona filamu hiyo mpya ya Ukwa, wakiamini itakuwa na vichekesho na vituko vya kuvunja mbavu.

1 comment: