KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 30, 2012

KINNAH PHIRI: Wanasoka wa Tanzania hawajiamini

WAKATI kikosi cha timu ya soka ya Taifa Stars kimeondoka nchini leo kwenda Ivory Coast, Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Malawi, Kinnah Phiri amesema tatizo kubwa la wanasoka wa Tanzania ni kutojiamini. Phiri alisema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita mara baada ya Taifa Stars kutoka suluhu na Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika makala hii ya ana kwa ana iliyoandikwa na ATHANAS KAZIGE, kocha huyo anaelezea masuala mbalimbali kuhusu kikosi cha Taifa Stars.
SWALI: Timu yako ya soka ya taifa ya Malawi leo imecheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Taifa Stars. Ni kipi ulichokibaini kwa Taifa Stars katika mechi hiyo?
JIBU: Kwanza kabisa napenda kumpongeza kocha mpya wa Taifa Stars, Kim Poulsen kwa kupewa kazi ya kuinoa timu hiyo, kuchukua nafasi ya Jan Poulsen, ambaye niliwahi kukutana naye katika mechi kama hii.
Kwa ujumla, mtindo aliokuja nao Kim unaonyesha wazi kuwa, ana mwelekeo mzuri kwa kuita vijana wengi, ambao ndio damu changa kwenye kikosi, lakini nina hakika kwamba atakumbana na changamoto nyingi.
Changamoto hizo ni pamoja na kupigiwa kelele nyingi kutoka kwa mashabiki, hasa wale ambao wanapenda maendeleo ya haraka na kusahau kwamba mchezo wa soka unahitaji kuwekezwa mapema kwa kuwaandaa vijana tangu wakiwa wadogo.
Kitu kingine muhimu kwa watanzania kukitambua ni kwamba, kocha yeyote anapokabidhiwa timu kwa mara ya kwanza, ni lazima ichukue muda mrefu kwa wachezaji kuuelewa mfumo wake na kucheza anavyotaka. Hii ni kwa sababu wachezaji wameshazoea kucheza kwa mfumo waliofundishwa na kocha wa zamani.
Ni kweli katika kikosi cha sasa cha Taifa Stars wapo wachezaji wachache waliofundishwa na Jan Poulsen, lakini inawezekana kabisa kuwa, mfumo aliokuja nao Kim Poulsen ni tofauti, licha ya wote wawili kutoka nchi moja ya Denmark.
Katika mazingira haya, ni wazi kwamba zitajitokeza kasoro hizi na zile kwenye timu ya Taifa Stars, lakini baada ya wachezaji kuzoea, bila shaka mambo yanaweza kubadilika.
SWALI: Umegundua kasoro ipi kwa wachezaji wa Taifa Stars baada ya kucheza nao mechi ya leo?
JIBU: Tatizo pekee kubwa nililolibaini kwa wachezaji wa Taifa Stars ni kutojiamini wanapokuwa uwanjani. Inawezekana tatizo hili limetokana na mashabiki kuwazomea kwa vile siku zote mashabiki wanataka timu inapocheza nyumbani, ifanye vizuri.
Na ilivyo kawaida ni kwamba, mchezaji anapozomewa na mashabiki wake, anavunjika nguvu haraka kutokana na kuathirika kisaikolojia na ni rahisi kwa timu nzima kupoteana na kupoteza mchezo. Hivyo ndivyo ilivyotokea kwa baadhi ya wachezaji, hawakuwa wakijiamini na ndio sababu kila mmoja alicheza kwa kutumia kipaji chake badala ya mfumo unaoeleweka.
Pamoja na kujitokeza kwa dosari hizo, nina hakika iwapo Taifa Stars itapewa muda zaidi, itakuwa na kikosi kizuri kwa sababu mafanikio yoyote katika soka, hayawezi kupatikana ndani ya wiki mbili ama mwezi mmoja.
SWALI: Malawi inakwenda kucheza na Uganda katika mchezo wa kusaka nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia za 2014. Nini maoni yako kuhusu uwezo wa kikosi chako?
JIBU: Kwanza nimefurahi sana kupata mechi moja ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars kwa sababu ni moja ya timu nzuri na ninazoziheshimu. Sikutarajia iwapo Taifa Stars ingekuwa na wachezaji wengi vijana na wazuri kwa sasa. Kwa maana hiyo, nimepata kipimo kizuri sana.
Zipo kasoro chache zilizojitokeza kwenye kikosi changu baada ya kucheza mechi hiyo. Miongoni mwa kasoro hizo ni wachezaji wangu wa safu ya kiungo na ushambuliaji kujisahau. Nitalifanyia kazi tatizo hilo baada ya mechi yetu inayofuata dhidi ya Zanzibar na nina hakika hadi siku tutakapocheza na Uganda, mambo yatakuwa mazuri.
Jambo la msingi ni kwamba kikosi changu nacho kinaundwa na wachezaji wengi wapya na vijana waliochanganyika na wakongwe. Nina hakika baada ya kuelewana vyema, wataweza kuifikisha nchi yetu mbali katika mashindano haya makubwa duniani.
SWALI: Unatoa ushauri gani kwa Taifa Stars ili iweze kufanya vizuri katika mechi yake dhidi ya Ivory Coast itakayochezwa mwezi ujao?
JIBU: Ushauri wangu kwa Taifa Stars ni kwamba, iwapo watapata mazoezi ya pamoja kwa muda mrefu na kufuata mafunzo ya kocha wao, wataweza kufanya vizuri katika mechi yao dhidi ya Ivory Coast. Jambo la msingi kwa wachezaji ni kujiamini na kuondoa woga wa kukumbana na wachezaji wenye majina makubwa duniani. Wakifanya hivyo, nina hakika kazi ya kukabiliana na Ivory Coast haitakuwa kubwa. Lakini wakicheza kinyume na hapo. huenda mambo yakawa magumu kwao.
Kama ulitazama vizuri mechi yetu dhidi ya Taifa Stars, tuliwazidi sana kimchezo,hasa kipindi cha pili, ambapo walionekana kuchoka na kutoa nafasi kwa timu yangu kufanya mashambulizi mengi. Inawezekana wachezaji wa Taifa Stars hawakupewa mazoezi ya kuongeza pumzi na kupeana pasi za uhakika ndio sababu walipoteza mipira mingi. Mara nyingi badala ya kusukuma mashambulizi mbele, walirudisha mipira nyuma.
Sote tunafahamu kwamba Ivory Coast inaundwa na wachezaji karibu wote wanaocheza soka ya kulipwa barani Ulaya na wenye majina makubwa. Hivyo wachezaji wa Taifa Stars wakicheza kwa kuhofia majina hayo, wanaweza kupata matatizo. Lakini wakiwaona ni sawa kama wao, wanaweza kupata matokeo mazuri ugenini. Ni kweli kwamba Didier Drogba na Solomon Kalou wana uwezo mkubwa kwa kupiga chenga na kuwatoka mabeki wa timu pinzani, lakini ukiwabana kisawasawa, ni rahisi kuwadhibiti. Tatizo ni kwamba, ukiwapa nafasi moja tu, ni rahisi kwao kuitumia vizuri kupata bao.
Kitu kingine muhimu ni kwamba wachezaji wa Taifa Stars hawapaswi kuwa na papara wanapoingia kwenye lango la timu pinzani, hali inayosababisha wapoteze mipira mingi. Nina hakika kocha mwenzangu amelibaini tatizo hilo na atalifanyia kazi.
Cha msingi ni kwamba katika soka lolote linaweza kutokea. Kama wachezaji wa Taifa Stars watadhamiria kwa dhati kuishangaza dunia, hilo linaweza kutokea.
SWALI: Kwenye kikosi chako cha Malawi umejaza wachezaji wengi wanaocheza soka ya kulipwa nje. Unadhani hiyo ni njia nzuri ya kuiwezesha timu yako kufanya vizuri katika michuano hii?
JIBU: Nilichojaribu kukifanya ni kuwa na wachezaji wengi wenye uzoefu wa soka ya kimataifa kuliko kutegemea vijana pekee. Lakini asilimia kubwa ya wachezaji wangu ni vijana waliotapakaa katika nchi mbalimbali za kusini mwa Afrika, ambako wanacheza soka ya kulipwa.
SWALI: Unazungumziaje kuhusu vipaji kwa wanasoka wa Tanzania? Unadhani vipo vipaji vya kutosha?
JIBU: Ndio. Ni kweli wachezaji wengi wa Tanzania wana vipaji vya kucheza soka, lakini tatizo kubwa ni kutojiamini na ndio sababu utaona kuwa, idadi ya wachezaji wa Tanzania wanaocheza soka ya kulipwa nje ni ndogo ikilinganishwa na Malawi.

BENDI MPYA YAANZISHWA DAR

BENDI mpya ya muziki wa dansi ya WK Music Sound mwishoni mwa wiki iliyopita ilifanya onyesho la utambulisho wake lililofanyika kwenye ukumbi wa Pentagon uliopo Kurasini, Dar es Salaam. Bendi hiyo inaundwa na wanamuziki wengi maarufu kutoka bendi mbalimbali za mjini Dar es Salaam. Pichani, baadhi ya wanamuziki wa bendi hiyo wakiwajibika stejini wakati wa onyesho hilo. (Picha na Emmanuel Ndege).

FLAVIANA: Serikali iwathamini wasanii

MWANAMITINDO nyota wa Tanzania, Flaviana Matata ameitaka serikali itambue umuhimu wa kazi za wasanii kutokana na juhudi zao binafsi za kuitangaza nchi kimataifa.
Flaviana amesema itakuwa haina maana kwa msanii kusifiwa kutokana na kazi zake nzuri baada ya kifo chake kama ilivyotokea kwa aliyekuwa msanii nyota wa filamu nchini, marehemu Steven Kanumba.
Akizungumza na mtandao wa filamucentral hivi karibuni, Flaviana alisema kifo cha Kanumba kilionyesha ni jinsi gani wasanii wanavyokubalika katika jamii na hata nje ya mipaka ya Tanzania.
“Tazama wasanii kama AY (Ambwene Yesaya), mtu kama Hasheem Thabeet na wengineo, serikali inawaunga mkono kwa kiwango gani katika kulitangaza Taifa hili? Lakini katika kifo cha Kanumba, tulimwona kila kiongozi alifika msibani,”alisema Flaviana.
Flaviana aliitaka serikali iache kuelekeza nguvu zake katika mchezo wa soka na mingineyo, badala yake itupie macho fani zingine, ambazo zimesaidia kulitangaza jina la Tanzania kimataifa.
Mshindi huyo wa zamani wa taji la Miss Universe Tanzania alisema, licha ya juhudi zake binafsi za kuitangaza nchi kimataifa, alishangazwa kuona akiwekewa vikwazo kugomboa vifaa vya msaada alivyovileta nchini kwa ajili ya abiria wanaosafiri kwa meli.
Flaviana alisema alileta nchini maboya 500 kwa ajili ya msaada kwa wakazi wa kanda ya ziwa, ikiwa ni kumbukumbu ya watu waliopoteza maisha kutokana na ajali ya meli ya MV Bukoba.
“Nilikabiliana na mtihani mkubwa baada ya kuambiwa nilipie kodi mara tano ya bei ya manunuzi,”alisema kwa mshangao mrembo huyo, asiyejichubua wala kubadili rangi ya ngozi yake.
Kanumba alifariki dunia Aprili 7 mwaka huu nyumbani kwake Sinza Vatican, Dar es Salaam na inasemekana kifo chake kilitokana na kusukumwa na msanii mwenzake, Elizabeth Michael ‘Lulu’.

P-SQUARE WAFANYA KUFURU









Wanunua ndege ya kusafiria aina ya airbus
Waingizwa kwenye klabu ya mabilionea Nigeria
LAGOS, Nigeria
WANAMUZIKI ndugu wawili mapacha wa kundi la P Square la Nigeria, Peter na Paul Okoye hivi karibuni walidhihirisha kuwa, pesa kwao si tatizo baada ya kununua ndege yao binafsi ya kusafiria.
Habari za uhakika zimeeleza kuwa, peter na Paul wametumia mamilioni ya dola kununua ndege hiyo aina ya airbus kutoka katika moja ya kampuni za Arabuni.
Peter na Paul wanatajwa kuwa ndio wanamuziki tajiri kuliko wote nchini Nigeria kwa sasa, wakiwa wamerekodi na kuuza albamu kadhaa sehemu mbalimbali duniani.
“Tumenunua ndege yetu ya kusafiria. Asante Mungu na mashabiki. Nyote mmewezesha hili lifanikiwe,” alieleza Peter kupitia kwenye mtandao wa Twetter.
Wanandugu hao, ambao wamekuwa wakitengeneza pesa nyingi kupitia muziki, pia wanamiliki mali mbalimbali katika miji ya Jos na Port Harcout, likiwemo jumba la kifahari lenye thamani ya Naira milioni 400 lililopo katika mji wa Lagos.
Wanamuziki hao pia wanamiliki magari ya kifahari aina ya Sequioa Sports Utility Vans (SUVs), Toyota Altima na mengineyo kadhaa.
Wachambuzi wa masuala ya muziki wameeleza kuwa, Peter na Paul kwa sasa wameingizwa kwenye klabu ya mabilionea nchini Nigeria kutokana na uwezo mkubwa wa kipesa walionao.
Historia ya P-Square inaanzia katika shule ya sekondari ya St Murumba, inayomilikiwa na Kanisa Katoliki mjini Jos, Nigeria. Wakiwa shuleni hapo, walijihusisha zaidi masuala ya muziki na ngoma za kiasili na kuanza kuimba nyimbo za wanamuziki maarufu wa Marekani kama vile MC Hammer, Bobby Brown na Michael Jackson.
Baadaye, mapacha hao waliunda kundi lililojulikana kwa jina la MMMPP, ikiwa ni vifupisho vya majina ya Itemoh, Michael, Melvin, Peter na Paul.
Kutokana na kuvutiwa na muziki wa Michael Jackson, waliamua kujikita katika uchezaji wa miondoko ya break dance na kuunda kundi la Smooth Criminals mwaka 1997.
Mwaka 1999, Peter na Paul waliamua kurejea katika shule ya muziki kwa ajili ya kuendeleza vipaji vyao katika upigaji wa kinanda, drums na magita ya besi na rhythm. Nyimbo walizopiga zilitumika katika filamu kadhaa za Kinigeria kama vile Tobi, Mama Sunday, Moment of Bitterness na Evas River.
Mwaka huo huo, mapacha hao waliamua kuunda kundi lao la Double P kabla ya kubadili jina na kujiita P-Square. Kazi zao zinasimamiwa na Bayo Odusami, maarufu zaidi kwa jina la Howie T, promota maarufu nchini Nigeria na Mkurugenzi wa Kampuni ya Adrot Nigeria Limited.
Mwaka 2001, P-Square walishinda shindano la Grab Da Mic na kampuni ya Benson & Hedges iliamua kudhamini albamu yao ya kwanza, inayojulikana kwa jina la Last Nite, iliyotolewa chini ya lebo ya Timbuk2.
Miezi mitatu baada ya kutoa albamu hiyo, kundi la P-Square lilishinda tuzo ya kundi linalochipukia kimuziki barani Afrika katika tuzo za Kira.Pia walishinda tuzo ya kundi bora la muziki wa R&B mwaka 2003.
Mwaka 2005, P-Square walitoa albamu yao ya pili, inayojulikana kwa jina la Get Squared chini ya lebo yao, Square Records. Albamu hiyo ilisambazwa na Kampuni ya TJoe Enterprises. Video za albamu hiyo zilishika namba moja kwa wiki nne mfululizo katika MTV Base.
P-Square wana mashabiki wengi zaidi nchini Afrika Kusini, hasa katika mji wa Cape Town. Wamewahi kufanya maonyesho na wanamuziki mbalimbali maarufu duniani kama vile Ginuwine, Sean Paul, Akon na Busola Keshiro.
Mwaka 2007, kundi hili lilitoa albamu yao ya tatu, ambayo ndiyo inayoongoza kwa mauzo. Albamu hiyo, inayojulikana kwa jina la Game Over, iliuzwa nakala milioni nane sehemu mbalimbali duniani.
Albamu yao ya nne inayojulikana kwa jina la Danger ilitoka mwaka 2009. Ndani ya albamu hiyo, walirekodi baadhi ya nyimbo zao kwa kushirikiana na wasanii wengine nyota kama vile 2face Idibia, J Martins na Frenzy.
Mwaka 2010, kundi hilo lilishinda tuzo ya wasanii bora wa mwaka katika tuzo za Kora zilizofanyika katika mji wa Ouagadougou, Burkina-Faso. Walitangazwa kuwa washindi wa tuzo hiyo wakati wakiwa London, Uingereza walilokwenda kufanya onyesho.

WEMA AVISHWA PETE NYINGINE YA UCHUMBA



Mwimbaji wa bendi ya muziki wa dansi ya Machozi, Mwinyi akimvalisha pete ya uchumba mwigizaji nyota wa wa filamu za bongo movie, Wema Sepetu wakati wa onyesho la bendi hiyo lililofanyika juzi kwenye ukumbi wa Maisha Club Jijini Dar es Salaam. (Picha/Dj Choka Blog).

MAKALLA: Kapambaneni, msiogope majina ya kina Drogba

SERIKALI imewataka wachezaji wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars kutoogopa majina ya wachezaji wa Ivory Coast, badala yake wawaone ni watu wa kawaida.
Mwito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla alipokuwa akizungumza na wachezaji wa timu hiyo wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya taifa.
Makalla alisema Ivory Coast inaundwa na wachezaji wa kawaida kama waliopo Taifa Stars na kama ni kuwazidi, wanaweza kufanya hivyo katika vitu vichache.
Alisema wachezaji wa Taifa Stars wanapaswa kuonyesha soka ya ushindani na kupata matokeo mazuri, yatakayowaweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014.
Taifa Stars inatarajiwa kuondoka nchini leo alfajiri kwenda Abidjan kwa ajili ya pambano lao dhidi ya Ivory Coast lililopangwa kufanyika keshokutwa mjini humo.
Makalla alisema wachezaji wa Taifa Stars wanao uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya wenzao wa Ivory Coast na kusisitiza kuwa, jambo la muhimu ni kuondoa hofu na kucheza kwa kujituma.
Alisema iwapo Taifa Stars haitapata matokeo mazuri katika mchezo huo, mashabiki wake watakasirika na kupunguza mapenzi yao kwa timu hiyo.
"Mnakwenda kucheza na timu, ambayo inaundwa na wachezaji wa kawaida kama nyinyi na mna uwezo wa kuwafunga, hivyo mkikutana nao onyesheni uwezo wenu na mbinu zenu, ambazo mmefundishwa na mwalimu wenu na mwisho mtafanikisha malengo yenu," alisema Makalla.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga alisema nidhamu na kujituma kwa wachezaji wa timu hiyo kutafanikisha ushindi na kuiweka Tanzania katika msimamo mzuri wa mashindano.
Tenga alisema anaamini wachezaji wa Taifa Stars watapambana vyema na kupata matokeo mazuri, ambayo ndiyo dhamira ya kila mtu na hapo ndipo mwanzo mzuri wa timu hiyo utakapoonekana baada ya kuanza kufundishwa na Kocha Kim Poulsen.
Kikosi cha Taifa Stars kilichoondoka leo alfajiri kinaundwa na makipa Juma Kaseja, Mwadini Ally na Deogratius Munishi. Mabeki ni Nassor Masoud Cholo, Aggrey Morris, Amir Maftah, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Waziri Salum, Shomari Kapombe na Juma Nyoso. Viungo ni Mwinyi Kazimoto, Salum Abubakar,Jonas Mkude , Shabani Nditi, Edward Christopher, Mrisho Ngasa na Frank Domayo wakati washambuliaji ni Mbwana Samata, Ramadhan Singano, Simon Msuva, Haruna Moshi na John Bocco.
Viongozi wanaofuatana na timu hiyo ni Kocha Poulsen, Sylvester Marsh (kocha msaidizi), Juma Pondamali (kocha wa makipa), Leopold Mukebezi (meneja wa timu), Juma Mwankemwa (daktari wa timu), Frank Mhonda (Physiotherapist) na Alfred Chimela (mtunza vifaa). Msafara huo unaongozwa na mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF, Crescentius Magori wakati naibu kiongozi wa msafara ni Makamu wa Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Haji Ameir Haji.

Kipingu yupo tayari kumrithi Nchunga Yanga

MWENYEKITI wa zamani wa Baraza la Michezo Nchini (BMT) na kilichokuwa Chama cha Soka nchini (FAT), Luteni Kanali mstaafu, Iddi Kipingu ni miongoni mwa wanachama wanaopigiwa debe Yanga kuwania nafasi ya mwenyekiti.
Kipingu amekuwa akipigiwa debe na wanachama wengi wa Yanga kuwania wadhifa huo kutokana na uzoefu mkubwa alionao katika uongozi wa michezo.
Mbali na uzoefu, sifa nyingine inayowafanya wanachama wa Yanga wampigie debe Kipingu kuwania wadhifa huo ni uadilifu na msimamo wake katika uongozi.
Baadhi ya wanachama wa Yanga waliozungumza na Burudani wiki hii mjini Dar es Salaam walisema, Kipingu ndiye mwanachama pekee mwenye uwezo wa kuitoa klabu hiyo ilipo sasa na kuifikisha mbali.
Wanachama wengine, ambao wamekuwa wakipigiwa debe kuwania wadhifa huo ni pamoja na mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo, Francis Kifukwe na makamu wenyeviti wa zamani, Mbaraka Igangula na Davis Mosha.
Akizungumza na Burudani kwa njia ya simu jana, Kipingu alithibitisha kupokea maombi hayo kutoka kwa wanachama wengi wa Yanga, lakini alisema bado anatafakari.
Fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi Yanga zinatarajiwa kuanza kutolewa keshokutwa wakati uchaguzi mkuu wa klabu hiyo umepangwa kufanyika Julai 15 mwaka huu.
Kipingu alisema kwa sasa hawezi kuamua iwapo atagombea nafasi hiyo kutokana na sababu mbalimbali. Alizitaja baadhi ya sababu hizo kuwa ni pamoja na kutojua vyema tatizo linaloikabili Yanga kwa sasa.
"Naweza kusema nipo tayari kugombea nafasi hiyo, lakini kwanza nataka kiitishwe kikao cha wadau wa Yanga ili tujadiliane kwanza tatizo ni nini kabla ya mimi kuchukua fomu,"alisema Kipingu.
Alisema anapenda kuiona Yanga ikirejea katika hali nzuri na kumalizika kwa tofauti zote zilizojitokeza hivi karibuni miongoni mwa wanachama.
"Unajua uongozi ni ushirikiano. Napenda kuona tunakubaliana kwanza ndipo nichukue fomu. Nataka wawepo watu wote muhimu, wakiwemo wale wazee 20, wafadhili na viongozi wa zamani ili tuweze kuwekana sawa na tuwe na lengo moja, nami nitaingia,"alisema Kipingu.
Kwa sasa, Yanga haina uongozi wa kuchaguliwa baada ya aliyekuwa mwenyekiti, Lloyd Nchunga kuamua kujiuzulu, kutokana na shinikizo kubwa la wanachama na wazee wa klabu hiyo.
Kufuatia kujiuzulu kwa Nchunga, klabu hiyo kwa sasa ipo chini ya sekretarieti ya Yanga, inayoongozwa na Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa.

Airtel yaongeza zawadi katika promosheni ya Nani Mkali

Ofisa Uhusiano wa Airtel, Dangio Kaniki akifafanua jambo wakati wa mkutano wa
waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi ya kushiriki promosheni ya Nani Mkali
iliyoongezwa muda andika neno “Mkali” tuma kwenda 15656 bure. Baada ya hapo
atatumiwa maswali na kila atakapo toa jibu sahihi atapata pointi 20 na jibu
lisilo sahihi pointi 10.Kila ujumbe wenye jibu utatozwa shillingi 350 pamoja na
kodi. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeongeza muda kwa
wateja wake kuendelea kucheza promosheni yake kabambe ya Nani mkali
ambayo ilianza miezi mitatu iliyopita na kuwafaidisha zaidi ya wateja 90 wa
Airtel waliojishindia jumla ya miliono 217 kwa mgawanyo wa kuanzia milioni
1 kila siku, milioni 3 kila wiki na milioni 30 kwa washindi wa mwezi
Akiongea na waandishi wa habari leo, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania,
Jackson Mmbando alisema promosheni hii imekuwa na faida kwetu Airtel
wateja wetu waliokuwa wakishiriki wameifurahia na ndio maana leo
tumeamua kuongeza zawadi na muda wa promosheni ya Nani Mkali.
Hivyo promosheni yetu inaongezwa muda wa miezi miwili huku zawadi
zitakazo toka ni pesa taslim Jumla ya ya shilingi milioni 143 katika mgawanyo
wa kuanzia shilingi milioni 1 kila siku-washindi 52, milioni 3 kila wiki
–washindi 7,na milioni 30 kwa kila mwezi itatoka kwa washindi 2.
Pia tutakuwa na washindi wengine watakaogawana kitita cha shilingi milioni
10 za zaidi ikiwa watakuwa kati ya wachezaji bora wa promosheni ya Nani
mkali
Ili mteja kushiriki na kujishindia zawadi hizi kabambe Afisa Mawasiliano wa
Airtel bi Dangio Kaniki alisema,” kudhihirisha kauli mbiu yetu ya jisikie huru
katika promosheni hii mteja anatakiwa kuandika neno “Mkali” na kutuma
kwenye namba 15656 bure kabisa ili kujiunga. Baada ya hapo atatumiwa
maswali na kila atakapo toa jibu sahihi atapata pointi 20 na jibu lisilo sahihi
pointi 10.Kila ujumbe wenye jibu utatozwa shillingi 350 pamoja na kodi.
Promosheni hii pia itatoa fursa kwa wateja kuchagua lugha wanayotaka kwa
kutuma neno “swa” kwa Kiswahili au “eng” kwa lugha ya kiingereza kwenda
namba 15595 Kujua alama ulizonazo au point mteja wetu atatakia kutuma
neno “point” au “alama” kupatiwa pointi alizojikusanyia. Kujiondoa kwenye
promosheni mteja atatakiwa kutuma neno “cancel’ au “stop” kwenda namba
15595
Promosheni ya nani mkali ilizinduliwa rasmi februari 15, 2012 na kudumu kwa
muda wa miezi mitatu.Nani Mkali imefanikiwa kuwazawadia wateja wa Airtel
kutoa mikoa mbali mbali ikiwemo Arusha, Muheza Tanga and DSM, Tabora,
Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Kilimanjaroa na mingine mingi.

Tuesday, May 29, 2012

SPRITE YADHAMINI KLINIKI YA KIKAPU JIJINI DAR

Mchezaji maarufu wa mpira wa kikapu na anyechezea ligi ya NBA ya Marekani,
Hasheem Thabeet akiongea na waandishi wa habari (hawako pichani)
kuhusu kliniki ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Sprite itakayofanyika
katika viwanja vya Don Bosco, Upanga Dar es Salaam kuanzia Ijumaa Juni
Mosi 2012.


Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania
(TBF) Michael Maluwe akizungumza na waandishi wa habari (hawako
pichani)kuhusu ya kliniki ya vijanai chini ya umri wa miaka 17 itakayofanyika
katika viwanja vya Don Bosco, Upanga jijini Dar es Salaam kuanzia Ijumaa
Juni Mosi mwaka huu. Kliniki hiyo imedhaminiwa na Kampuni ya Coca-Cola
kupitia kinywaji cha Sprite. Katikati ni mchezaji wa Ligi maarufu duniani ya
NBA Hasheem Thabeet na kulia ni Meneja Bidhaa Msaidizi wa Coca-Cola
Tanzania Warda Kimaro.


Sprite, moja ya vinywaji maarufu vya kampuni ya Coca-Cola leo imetangaza
kudhamini kliniki ya mchezo wa kikapu kwa vijana chini ya umri wa miaka 17
itakayofanyika kwenye kiwanja cha Don Bosco, Upanga, jijini Dar es Salaam
kuanzia Ijumaa juni 1hadi June 2, chini ya mchezaji wa kimataifa wa mchezo
huo Hasheem Thabeet.
Zaidi ya vijana 200 kutoka mikoa sita watashiriki kliniki hiyo ambayo itatoa
mafunzo ya awali ya mchezo wa kikapu kama vile kumiliki mpira na kutoa
pasi. Katibu mkuu msaidizi wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu nchini Michael
Maluwe amesema kuwa washiriki watatoka mikoa ya Mwanza, Mbeya,
Dodoma, Kilimanjaro, Arusha, Unguja na Pemba.
“Tunashukuru kupata fursa hii ya mafunzo ya awali kwa vijana ambao kusema
kweli ndiyo uti wa mungongo wa maendeleo ya mchezo wa kikapu hapa
Tanzania”, amesema Maluwe na kupongeza juhudi zinazofanywa na Coca-Cola
kupitia Sprite za kudhamini shughuli za maendeleo ya mchezo wa mpira wa
kikapu.
Hii ni mara ya pili kwa Sprite kudhamini kliniki ya kikapu kwa vijana chini ya
ukufunzi wa Hasheem Thabeet. Kliniki kama hii ilifanyika mwaka 2010 kwenye
uwanja huo huo wa Don Bosco na kushirikisha zaidi ya vijana 200 kutoka Dar
es Salaam na mikoa mengine.
Thabeet ni nembo ya mafanikio katika mchezo wa mpira wa kikapu na ni
mchezaji pekee kutoka Tanzania kuwahi kucheza kwenye ligi maarufu duniani
ya NBA. “Najisikia fahari kupata fursa kama hii, kwa mara nyingine tena, ili
kuweza kuwafundisha na kuwahamasisha vijana kucheza mpira wa kikapu.
Naamini baadhi yao watachomoza kuwa wachezaji nyota siku za usoni”,
alisema Thabeet ambaye yuko nchini tayari kuendesha kliniki hiyo.
Kwa upande wake, Meneja Mzaidizi Bidhaa wa Coca-Cola Tanzania Warda
Kimaro amesema: “Sprite inajisikia furaha kupata nafasi hii ya kusaidia
maendeleo ya mchezo wa kikapu na tunaamini kwamba kliniki hii ya Hasheem
Thabeet itawasaidia vijana kuelewa vitu msingi katika maendeleo ya mchezo
wa mpira wa kikapu”.
Sprite ilianza kudhamini mchezo wa mpira wa kikapu hapa nchini tangu
mwaka 2010 na tangia hapo imeweza kudhamini shughuli mbali mbali za
kikapu ikiwa ni pamoja na mashindano ya vijana mikoani, mashindano ya
kanda ya tano, mechi za timu ya Marekani AND1 ambao walikuwa hapa nchini
mwezi uliopita na kucheza mechi za kirafiki katika mikoa ya Mwanza, arusha
na Dar es Salaam kwa udhamini wa Sprite.
Mbali na kudhamini mashindano, Sprite pia imesaidia kuboresha viwanja wa
mchezo wa mpira wa kikapu katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Dodoma,
Mbeya, Mwanza, Arusha na Kilimanjaro.

Airtel yakabidhi vifaa vya michezo kwa DRFA

Ofisa Uhusiano wa Airtel Tanzania,Jane Matinde akisisitiza jambo wakati
akiongea na waandishi wa habari (hawako pichani) wakati wa kukabidhi vifaa
vya michezo kwa timu za shule za sekondari zitakazoshiriki michuano ya Airtel
Rising Stars ambayo inatarajiwa kuanza kesho,jumatano Mei 30.



Ofisa Uhusiano wa Airtel Tanzania,Jane Matinde akimkabidhi jezi Katibu Mkuu wa
chama cha mpira mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) wakati kampuni ilipokabidhi
vifaa vya michezo kwa timu za shule za sekondari zitakazoshiriki michuano ya
Airtel Rising Stars ambayo inatarajiwa kuanza kuanza kesho,Jumatano Mei 30.



Airtel Tanzania jana ilikabidhi vifaa vya michezo kwa timu za shule za
sekondari 24 zitakazoshiriki kwenye michuano ya vijana wenye umri chini ya
miaka 17 maarufu kama Airtel Rising Stars ambayo inatarajiwa kuanza
kutimua vumbi kesho Mei 30, ngazi ya Mkoa.
Shule zitakazoshiriki kwenye michuano hiyo ni zile zilizofanya vyema kwenye
michuano ya shule za sekondari (UMISSETA), ambazo ni Lindi sekondari,
Mpunyule na Nkowe zote za Mkoa wa Lindi, Southern Highland, Mbeya Day na
Wenda Sekondari kutoka Mbeya.
Nyingine ni Mbande Sekondari, Kurasini na Kiravi (Temeke), Airwing,
Benjamini Mkapa na Msogola Sekondari (Ilala), Twiga Sekondari, Goba na
Makongo Sekondari (Kinondoni), Sinoni, Kaloleni na Bishop Durning (Arusha).
Timu hizo zote zimethibitisha ushiriki wao na kuahidi kufanya vizuri ili
kushinda mechi zao. Mechi za mikoa zitatumika kuchangua timu kombaini
zitakazowakilisha mikoa kwenye mashindano ya Airtel Rising Stars ngazi ya
taifa yatakayoanza Juni 9 mpaka Juni 17 Jijini Dar es Salaam.
Wakati timu za wavulana zikatarajiwa kushindana kwenye ngazi ya mkoa ili
kuchanguliwa kucheza michuano ya Taifa, timu moja kutoka kila Mkoa itafuzu
moja kwa moja na kufanya timu zitakazoshiriki ngazi ya taifa kuwa 12, sita za
wavulana na sita wasichana.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar
es Salaam leo, Meneja Masoko na Matangazo Airtel Tanzania Rahma
Mwapachu alisema Airtel inajivunia ushirika wake na moja ya Klabu kubwa
duniani - Machester United, kuinua kiwango cha mpira wa miguu nchini
Tanzania na Afrika.
'Tunaamini ya kuwa kwa ushirikiano wetu na Manchester United na TFF
tutakuza kwa kiasi kikubwa kiwango cha mpira wa miguu hapa nchini
Tanzania. Tunaamini vijana wakiandaliwa vizuri wanaweza'.Mwapachu
alishukuru Wizara ya Habari, Vijana, Utamanduni na Michezo kwa ushirikiano
wanaotoa ili kukuza mpira hapa nchini.
Airtel Rising Stars ni mpango kabambe wa Afrika nzima ambao ni kuibua na
kukuza vipaji vya wanasoka wanaochipukia, wavulana na wasichana wenye
umri wa miaka chini ya kumi na saba ambao watapata muda muafaka wa
kuonyesha vipaji vyao na kukutana na waatalum wa mpira wa miguu na
kupata mafunzo zaidi hivyo kukuza vipaji vyao.
Mwaka jana, Klabu ya Manchester United ilitoa walimu wake wa soka la vijana
kufundisha kliniki za soka za kimataifa zilizofanyika Tanzania, Afrika Kusini na
Gabon ambapo walishiriki walipata nafasi ya kufundisha jinsi ya kucheza mpira
wa miguu kwa mtindo wa Manchester United.
Kliniki ya aina hiyo itafanyika Jijini Nairobi Agosti mwaka huu kwa nchi
zinazozungumza Kingereza Tanzania ikiwemo. Nairobi pia itakuwa mwenyeji
wa mashindano ya Airtel Rising Stars inter-continental ambayo itashirikisha
nchi 14 ambapo Airtel inafanya biashara. Tanzania itawakilishwa na mshindi
wa fainali za taifa pamoja na wachezaji sita bora, watatu wavulana na watatu
wasichana.

Meneja aliyetimuliwa Twanga Pepeta atua Mashujaa

Aliyekuwa Meneja wa bendi ya Twanga Pepeta International, Martine Sospeter (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi kuhusu uamuzi wake wa kujiunga na bendi ya Mashujaa. Kushoto ni kiongozi na mwimbaji wa bendi hiyo, Charlz Baba na kulia ni mratibu na mwanzilishi, Dodoo La Bouche.


"Juzi usiku nilishangazwa na kauli ya mkurugenzi wangu wa zamani katika
Bendi ya African Stars,Asha Baraka katika vyombo mbalimbali vya habari
kuwa amenifukuza kazi kutokana kuhujumu bendi ikiwemo kushawishi
wanamuziki kujiunga na bendi ya Mashujaa.
Kwa kweli kauli ile ilinisikitisha sana kutokana na ukweli kwamba Asha
nilimchukulia kama dada yangu,kwani nilifanya naye kazi kwa miaka 14 iweje
hii leo aje anitolee maneno ya kunichafua katika vyombo vya habari?
Mimi sijawahi kuhusika na mpango wowote wa wasanii wa Twanga kuhamia
Mashujaa na wala sikuwa nafahamu mpango huo zaidi ya mwisho wa siku
kusikia fununu za chinichini na mwishowe wasanii hao kutangazwa kuhamia
Mashujaa.
Leo napenda nitangaze rasmi kwamba nimeachana na African Stars na
kujunga na Mashujaa Entertainment na tayari nimeshasaini mkataba wa kazi
katika bendi hii".
“Nilipanga nifanye taratibu za kumuaga kutokana na kuwa nilikuwa nafanya
kazi kwake bila ya mkataba lakini nimepata bendi hii ambayo tulikaa na
kukubaliana mambo mbalimbali.
Mbali na mkataba baadhi ya makubaliano na uongozi wa mashujaa ni pamoja
na kunipangia nyumba hali itakayoniladhimu kuhama ile iliyokuwa chini ya
Twanga.
Ninaamini nitafanya vema kazi yangu hii mpya kama ilivyokuwa Twanga
ambapo nilidumu kwa muda mrefu na kuchangia kufika hadi hapo nilipoachia,
hivyo naomba ushirikiano kwa uongozi, wanamuziki, Wadau na hata ninyi
mwaandishi wa habari."
Mwisho wa taarifa.

Monday, May 28, 2012

Utata wa umri wa Lulu kuamriwa Juni 16



Mahakama Kuu kanda ya Dar es salaam imepanga kutoa uamuzi juu ya umri wa msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba Aprili 7 mwaka huu.

Jaji Fauz Twaib leo alisikiliza mapingamizi ya mawakili wa serikali kuhusiana na maombi ya mawakili wanaomtetea Lulu waliyowasilisha mahakamani hapo kuiomba korti hiyo aidha ichunguze umri wa Lulu anayedai ana miaka 17 au iamuru mahakama ya kisutu kuchunguza.

Baada ya kuwasilishwa maombi hayo leo ilikuwa ni siku ya kusikilizwa maombi mahakamani ambapo wakili Shadrack Kimaro wa Serikali alipinga vikali maombi hayo kuwepo mahakamani hapo akidai kuwa hayakustahili kuwepo na badala yake yatupwe.

Alidai walichofanya ni kinyume cha sheria ilipaswa wakate rufaa kwasababu maombi yalishafika mahakama ya kisutu inakosikilizwa kesi hiyo na kutolewa maamuzi hivyo haikuwa sahihi kufungua maombi mapya wakati sio maombi mapya.

Aliwashauri mawakili wa Lulu aidha kukata rufaa maamuzi ya Kisutu au kuomba maamuzi yale kufanyiwa mapitio. Hata hivyo alidai kifungu cha sheria kilichotumika kuwasilisha maombi hayo sio sahihi ilipaswa kitumike kifungu ambacho kitaipa mamlaka korti hiyo kusikiliza maombi.

Mawakili wa Lulu, Furgence Masawe, Peter Kibatala na Kennedy Fungamtama hawakukubaliana na hayo,ambapo Fungamtama aliiomba mahakama kupokea maombi yao na kutolea uamuzi kwasababu ndiko maombi yao yanakotakiwa kupelekwa.

Aliusoma upya uamuzi uliotolewa Kisutu na kudai kuwa haukuwa uamuzi bali maelekezo ya mahakama na wao wamefata maamuzi hayo yaliyowataka kuwasilisha maombi yoyote Mahakama Kuu kwasababu mahakama ile haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mauaji.

Baada ya kusikiliza mabishano hayo ya kisheria mahakama hiyo imepanga kutoa maamuzi Juni 16 mwaka huu.

Airtel Jiunge na Supa 5 yapasua anga mkoani Dodoma

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (kushoto) akikabidhi
zawadi ya simu kwa, Baltazar Theobald, mshindi wa kwanza aliyeweza kueleza
vizuri jinsi ya kujiunga na huduma mpya ya Airtel Jiunge na Supa 5 wakati wa
hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Airtel
Jiunge na Supa 5 Ilizinduliwa kwa mara ya kwanza jijini Dar es Salaam hivi
karibuni.


Wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa kundi la Wanaume Family, Said
Juma ‘Chege’ (kushoto) na Amani James Temba ‘Mheshimiwa
Temba’wakionyesha makali yao katika onyesho la uzinduzi wa huduma ya
Airtel Jiunge na Supa 5 mjini Dodoma mwishoni mwa wiki



Mpiga tumba mahiri wa bendi ya Mashujaa Musica aliyejiunga na bendi hiyo akitokea
Twanga Pepeta, Sudi Mohamed ‘MCD’ akionyesha makali yake wakati wa
onyesho la uzinduzi wa huduma ya Airtel Jiunge na Supa 5 mjini Dodoma
mwishoni mwa wiki.



Rais wa Bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel Cyprian ‘ Chaz Baba’ ambaye naye amehama akitokea Twanga Pepeta, akiimba wakati wa onyesho la uzinduzi wa huduma ya Airtel Jiunge na Supa 5 mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.



Msanii wa kundi la muziki wa bongo fleva la Tip Top Connection lenye maskani yake mitaa ya Manzese jijini Dar es Salaam Hamad Ally ‘Madee’ akichengua mashabiki wake waliojitokeza katika onyesho la uzinduzi wa huduma ya Airtel Jiunge na Supa 5 mjini Dodoma mwishoni
mwa wiki.


Huduma ya SUPA 5 imepokelewa kwa shangwe mkoani Dodoma huku
dhamira yake ikiendelea kutimia baada ya umati mkubwa wa vijana kujitokeza
ili kufahamu vyema huduma hiyo nafuu iliyozinduliwa wiki moja iliypota kwa
lengo la kuwapa unafuu wateja wa Airtel ili kufurahia huduma tano nafuu
Wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika tamasha la wazi katika viwanja vya
Barafu mjini Dodoma wasanii wa muziki wa Dansi na Bongo Flaver
walitumbuiza na kufanya tamasha hilo kufana zaidi
Miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye utambilisho wa huduma hiyo
mpya kabambe ni pamoja na bendi ya muziki ya mashujaa, kundi la muziki
wa kizazi kipya la Tiptop Connection na kundi la Wanaume TMK.
Akitambilisha huduma hiyo mbele ya wakazi wa mji wa Dodoma na vitongoji
vyake Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando amesema, wateja wa
kampuni hiyo watapata unafuu mkubwa wa gharama za kupiga simu
“Huduma ya SUPA 5 inamuwezesha mteja wa Airtel kutumia mtandao wa
facebook bure masaa 24, kuongea nusu shilingi na watu watatu, kupiga simu
kwa robo shilingi kuanzia saa 4 usiku hadi saa 12 asubuhi na kutumia huduma
ya internet bure usiku kucha” alieleza Bw, Mmbando
Huduma ya SUPA 5 itaendelewa kutambulishwa katika mikoa mbali mbali kwa
kuwa huduma hiyo nafuu ni ya kudumu, mikoa inayotarajiwa kutembelewa
kwa kufanyiwa utambulisho rasmi wa huduma hiyo ya Airtel Supa 5 ni pamoja
na Morogoro, Iringa, Arusha, Mwanza na DSM.

MISS DAR INTER COLLEGE JUNI *

SHINDANO la kumsaka Miss Dar Intercollege 2012 linatarajiwa kufanyika Juni
8 kwenye ukumbi wa Sunciro, ulipo Sinza Shekilango jijini Dar es Salaam,
imefahamika.
Mratibu wa Shindano hilo Dina Ismail alisema jana kwamba warembo
watakaoshiriki shindano hilo wanaendeleza na mazoezi kwenye hoteli ya
Lamada jijini Dar es Salaam chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku
kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.

Alisema mpaka sasa warembo 12 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi
wa Habari (DSJ) na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha
(IFM) wamesharipoti kambini.

Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy
Maganga, Saada Seleman, Neema Nashon, Rose Muchunguzi, Fina
Revocatus,Jane Augustino,Theresia Issaya na Natasha Deo.

Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.

Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameyaomba makampuni mbalimbali
kujitokeza kudhamini shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na
hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.

“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano
letu. Mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania
(TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na
Clouds Fm.

MISS SINZA KUANZA KUJINOA JUNI MOSI

MAZOEZI ya warembo wataowania taji la Miss Sinza 2012 yamepangwa kuanza Juni Mosi kwenye ukumbi wa Ten Star Lounge (Mawela Social Hall) ulipo karibu na hotel ya Vatican City uliopo Sinza.
Mratibu wa mashindano hayo, Majuto Omary(pichani) alisema kuwa mazoezi hayo yataanza saa 10.00 jioni na ni ya wazi kwa warembo wenye nia ya kutaka kuwania taji na zawadi nono za washindi wa mwaka huu ambao wataiwakilisha Sinza kwenye mashindano ya Kanda ya Kinondoni, Miss Tanzania na baadaye katika mashindano ya Dunia “Miss World”.
Majuto alisema kuwa fomu za washiriki zitatolewa hapo hapo kwenye ukumbi wa mazoezi na wengine wanaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanatakiwa kufika ofisi za Mama Tike Hair Fashion and Boutique zilizopo Sinza Kumekucha kituoni, Ofisi za Miss Tanzania (Posta), ofisi za SMP zilizopo Kinondoni Mkwajuni, Brake Point (Kijitonyama na Posta) na kupitia mtandao wa balilemajuto.blogspot.com, sufiani mafoto.blogspot.com.
Alisema kuwa kamati ya Miss Sinza kwa sasa ipo katika mikakati mbali mbali ya kusaka wadhamini kwa ajili ya kufanikisha mashindano hayo yanayotarajiwa kuwa bora kabisa mwaka huu.
“Tunaomba wadhamini ikiwa ni makampuni, wafanya biashara, wadau wa masuala ya urembo ambao wanataka kujitangaza kupitia mashindano haya kujitokeza kusaidia waandaaji kwani lengo kubwa ni kuona Sinza inafanya mashindano bora na yenye kuleta mafanikio makubwa kwa kutwaa taji la Miss Tanzania na lile la Dunia,” alisema Majuto.
Alifafanua kuwa wameandaa mikakati na mipango mbali mbali ili kuhakikisha Sinza mwaka huu inapata mafanikio makubwa katika mashindano ya Miss Tanzania na yale ya Dunia.

DIAMOND AFANYA MAVITUZ BIG BROTHER AFRICA



Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' mwishoni mwa wiki iliyopita alionyesha machejo ya aina yake wakati alipopewa nafasi ya kutumbuiza katika hafla ya kutoka kwa washiriki wawili wa shindano la Big Brother Africa.



Kiwango Taifa Stars hakiridhishi

MWAMUZI Oden Mbaga akizungumza na mshambuliaji Haruna Moshi wa Taifa Stars wakati wa pambano la kirafiki la kimataifa dhidi ya Malawi lililochezwa juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka suluhu.



KIPA Juma Kaseja akipata maelekezo kutoka kwa Kocha Kim Poulsen wakati wa mechi hiyo.


TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars mwishoni mwa wiki iliyopita ilitoka suluhu na Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ilikuwa ya kuipima nguvu Taifa Stars kabla ya kuvaana na Ivory Coast katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014 itakayopigwa Juni 2 mwaka huu mjini Abidjan.
Licha ya kucheza nyumbani, Taifa Stars ilishindwa kuwapa burudani mashabiki wake kutokana na kuonyesha kiwango cha chini, tofauti na wapinzani wao, ambao walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo.
Hali hiyo ilisababisha baadhi ya mashabiki waliokosa uvumilivu, kuwazomea wachezaji wa Taifa Stars kila walipofanya makosa uwanjani na kuishangilia Malawi.
Uchezaji huo mbovu pia ulionekana kumchukiza kocha mkuu wa timu hiyo, Kim Poulsen ambapo kuna wakati aliinuka kwenye benchi na kuwafokea wachezaji wake kwa kuwanyoonyesha mikono akiwataka wapeleke mpira mbele.
Kilichompandisha hasira Kim ni kuona wachezaji wake kila mara wakirejesha mipira nyuma hata pale walipotakiwa kusukuma mashambulizi mbele, uchezaji ambao pia uliwafanya mashabiki wazomee.
Katika mechi hiyo, Taifa Stars ililifikia lango la Malawi mara nne na kupata nafasi nzuri za kufunga mabao, lakini umaliziaji mbovu wa washambuliaji wake ulikuwa kikwazo.
Kwa mfano, kuna wakati Mwinyi Kazimoto alitoa chumba safi kwa Mbwana Samatta aliyeingia na mpira ndani ya 18 kisha akatoa pasi iliyomgonga beki mmoja wa Malawi na kugonga mwamba wa pembeni wa goli.
Samatta na Mrisho Ngassa ni washambuliaji pekee waliokuwa wakijaribu kulazimisha mashambulizi kwenye lango la Malawi, lakini walishindwa kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa Haruna Moshi na Kazimoto.
Tatizo lingine kubwa lilijitokeza kwa baadhi ya wachezaji, ambao hawakuwa katika kiwango cha kawaida. Kwa mfano, haieleweki ni kwa nini kocha Kim alimpanga Kazimoto kucheza nafasi ya winga wa pembeni badala ya kiungo, ambayo ndiyo ameizoea.
Mchezaji mwingine aliyeonekana kucheza chini ya kiwango ni beki wa kushoto, Waziri Salum, ambaye alitolewa kipindi cha pili na nafasi yake kuchukuliwa na Amir Maftah.
Kiungo Shabani Nditi naye alifanya makosa mengi uwanjani ikiwa ni pamoja na kushindwa kuiunganisha vyema safu ya ulinzi na ushambuliaji na kutoa pasi butu ama kunyang’anywa mipira na wachezaji wa timu pinzani karibu na eneo la hatari.
Kiungo mwenzake, Frank Damayo naye hakuwa kwenye kiwango cha kawaida na haieleweki kwa nini kocha Kim alishindwa kumpumzisha katika kipindi cha pili kutokana na kutojiamini na pasi zake kupotea bure uwanjani.
Mabeki Kelvin Yondani, Aggrey Morris na Shomari Kapombe pamoja na kipa Juma Kaseja walionyesha uhodari mkubwa wa kuwazuia washambuliaji wa timu pinzani. Kama isingekuwa uhodari wa Kaseja, huenda Wamalawi wangepata hata mabao mawili.
Kilichowashangaza zaidi mashabiki waliohudhuria mechi hiyo ni kuona kocha Kim akishindwa kufanya mabadiliko mengine ya wachezaji katika kipindi cha pili.
Wakati Kocha Kina Phiri wa Malawi alifanya mabadiliko ya wachezaji watano, Kim alifanya mabadiliko ya mchezaji mmoja pekee. Hali hii ilisababisha maswali mengi kwa mashabiki iwapo kocha huyo hakuwa akijiamini.
Kwa maoni ya mashabiki wengi waliohudhuria mechi hiyo, Kim alipaswa kufanya mabadiliko ya wachezaji hata wanne ili kupima uwezo wao kwa sababu mechi hiyo ilikuwa ya kirafiki kwa lengo la kujipima nguvu.
Kitendo cha Kim kutofanya mabadiliko mengine zaidi kilitafsiriwa na baadhi ya mashabiki kuwa, kilionyesha woga wa kuhofia kufungwa nyumbani katika mechi yake ya kwanza. Huu ulikuwa udhaifu mkubwa kwa kocha huyo.
Baadhi ya mashabiki walisema ni bora kocha huyo angeingiza wachezaji wengine katika nafasi zilizopwaya ili aweze kupata kikosi cha kwanza kwa ajili ya kukabiliana na Ivory Coast.
Vinginevyo kama kocha huyo atakitegemea kikosi kilichocheza tangu mwanzo dhidi ya Malawi, Watanzania wasitarajie makubwa kutoka kwa Ivory Coast kwa sababu kilishindwa kucheza kitimu.
Pengine ni vyema kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuitautia Taifa Stars mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa ili Kim aweze kupata nafasi ya kupima wachezaji wengine na hatimaye kuwa na kikosi cha kwanza. Kim alikiri baada ya mchezo huo kuwa, kikosi chake kilikosa umakini na aliahidi kukifanyia marekebisho kabla ya pambano lao dhidi ya Ivory Coast. Ni marekebishi gani hayo? Tusubiri tuone.
Kikosi kilichocheza mechi hiyo ni kifuatacho: Juma Kaseja, Shomari Kapombe, Wazir Salum/Amir Maftah, Aggrey Morris, Kelvin Yondan, Shaban Nditi, Mrisho Ngasa, Frank Domayo, Mbwana Samatta, Haruna Moshi ‘Boban’ na Mwinyi Kazimoto.

Twiga Stars yachapwa mabao 2-1

TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, imeanza vibaya kampeni za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa kwa wanawake, baada ya kufungwa mabao 2-1 jioni hii mjini Addis Ababa na wenyeji, Ethiopia.

Twiga sasa inahitaji ushindi wa 1-0, Juni 16, katika mchezo wa marudiano mjini Dar es Salaam, ili kukata tiketi ya kucheza fainali hizo kwa mara ya pili mfululizo, Novemba mwaka huu, Equatorial Guinea, zikiwa ni za nane katika historia ya michuano hiyo

Uchaguzi Yanga Julai 15

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imeamua nafasi za
uongozi wa Yanga zilizoachwa wazi baada ya kujiuzulu viongozi mbalimbali
wa klabu hiyo zijazwe Julai 15 mwaka huu.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti
wa kamati hiyo, Deogratius Lyato ilieleza kuwa kutokana na mazingira hayo
Kamati ya Uchaguzi ya Yanga ianze mchakato huo wa uchaguzi kuanzia Juni mosi mwaka huu
kulingana na Katiba ya Yanga ibara ya 28 inayozungumzia nafasi iliyo wazi.
Lyato alisema Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliyokutana jana iliamua mchakato
huo uanze na uzingatie kikamilifu kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF
na kwamba nafasi zilizo wazi zitajazwa Julai 15 katika Mkutano wa uchaguzi
ambao mahali patapangwa na Kamati ya Uchaguzi ya Yanga kwa kushirikiana
na Sekretarieti ya klabu hiyo.
Alisema Mkutano wa Uchaguzi utakuwa na ajenda moja tu ya uchaguzi kujaza
nafasi zilizo wazi za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji wa kuchaguliwa na
kwamba Kamati ya Uchaguzi ya Yanga iandae na isimamie shughuli za
uchaguzi kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Yanga kwa mujibu wa kanuni za
uchaguzi za wanachama wa TFF chini ya usimamizi wa Kamati ya Uchaguzi ya
TFF na Katiba ya Yanga ibara ya 45(1) na (2).
Alisema hatua ya kuiagiza Yanga iitishe uchaguzi inatokana na kupata
ufafanuzi kutoka kwa Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF
iliyokutana juzi.
Kamati hiyo ya Sheria iliombwa kutoa mwongozo wa nini kifanyike ndani ya
Yanga baada ya wajumbe wake kadhaa kujiuzulu, hivyo Kamati ya Uchaguzi
ya Yanga ilikuwa imeomba mwongozo huo TFF.
Akitangaza muongozo huo kama walivyoombwa na Kamati ya Uchaguzi ya
Yanga mapema jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi kwa
Wachezaji ya TFF, Alex Mgongolwa alisema kujiuzulu kwa wajumbe wengi wa
Kamati ya Utendaji wa klabu hiyo kunawaondolea nguvu ya kimaamuzi
wajumbe waliosalia kwa mujibu wa Katiba ya klabu hiyo na kwamba kwa sasa
shughuli za uongozi wa klabu zitafanywa na Sekretarieti ya klabu hiyo mpaka
Mkutano Mkuu utakapoitishwa kujaza nafasi hizo.
Alisema Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Klabu hiyo ambao hawajatangaza
kujiuzulu ni pamoja na Salumu Rupia, Titto Ossoro, Sarah Ramadhani na
Mohamedi Bhinda hawana nguvu za kimaamuzi na hivyo hawawezi kuongoza
klabu hiyo mpaka mkutano mkuu utakapofanyika.
Mgongolwa alisema ili wajumbe hao wawe na nguvu ya kimaamuzi kwa
mujibu wa Katiba ya Yanga ni kwa idadi yao inapaswa kuwa asilimia 50 na
kwa sababu wajumbe waliojiuzulu ni wengi kuliko waliobakia, wanakosa
nguvu ya kimaamuzi.
Alisema hata wajumbe watatu walioteuliwa na Mwenyekiti wa Klabu hiyo kabla
hajajiuzulu ni batili kwa mujibu wa Katiba ya Yanga kwani uteuzi huo
unafanywa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ambapo idadi yao tayari
ilikuwa haikidhi kufanya uteuzi huo kwani wajumbe waliojiuzulu walikuwa
wengi.
Wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji ya Yanga walitangaza kujiuzulu
kuongoza klabu hiyo hivi karibuni akiwemo Mwenyekiti Lloyd Nchunga
kutokana na sababu mbalimbali.

Friday, May 25, 2012

Nchunga abwaga manyanga Yanga




Ndugu wana Habari, najua kwamba taarifa hii itawafedhehesha wajumbe na wanayanga wanaotuunga mkono,hasa ukizingatia maamuzi ya pamoja ya vikao vyetu vya kamati ya utendaji vilivyopita kwamba hakuna wa kujiuzulu kati yetu mpaka tujue hatma ya mkutano mkuu ambao tulipanga ufanyike tarehe 15 Julai 2012, ukiachia mbali shinikizo la kujiuzulu linalotolewa na baadhi ya wazee na wanaojiita vijana wa klab, kwa wajumbe wa kamati ya utendaji, na hasa mimi kama mwenyekiti.

Nawashukuru wajumbe kwamba tulifanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mzuri, na hata pale tulipotofautiana tulifanya hivyo kwa hoja na kufikia maazimio ambayo wote tulikuwa tunawajibika nayo.

Tangu tumeingia madarakani tumeweza kushirikiana na kupata mataji matatu katika kipindi cha mwaka mmoja, yaani; Ngao ya Hisani 2010, Ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2010/2011, na Ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup), 2011.

Zaidi ni kwamba tuliuwa uteja kwa watani wetu wa jadi kila tulipokutana katika ligi ukiachia mbali mechi ya tarehe 6 Mei 2012, ambayo tulifungwa goli 5 bila, na kuleta mtafaruku mkubwa katika klab yetu.Hali kadhalika tumeshirikiana mpaka tumeweza kuboresha mkataba kati yetu na TBL kupitia Kilimanjaro Premium Lager, tumeingia mkataba na kampuni ya NEDCO kuendeleza mali zetu katika mtaa wa mafia na uwanja wetu wa KAUNDA baada ya kufikia hatua nzuri katika kupata hati miliki za maeneo yote mawili.

Nafahamu kwamba kampuni hiyo iko katika hatua za mwisho za kumalizia michoro.Hali kadhalika tuliingia mkataba wa kuzalisha na kuuza bidhaa zenye nembo yetu na hasa baada ya kufanya marekebisho yatokanayo na matakwa ya sheria kule BRELA na pia mkataba na kampuni ya NEXUS LTD, ambayo itakuwa inatutafutia wadhamini wa nje na ndani, kufanya promosheni zetu na kampeni kwa njia ya electronic kupitia mitandao mbalimbali na kukusanya data za wanachama na kusajili wapya tukiwa na malengo ya kukusanya shilingi 300,000,000/= hadi 800,000,000/= kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitatu.

Haya yote tuliyafanya tukilenga kujitegemea kujazia mapengo yaliyokuwa yakitokana na kutegemea ufadhili wa mtu mmoja mmoja.Kwa ridhaa yenu tumekua tukiendelea na mazungumzo na makampuni mbali mbali kwa ajili ya udhamini na kwa sababu maalum, nitazitaja katika hati ya makabidhiano kwa kiongozi ajaye.

Aidha, tumeshirikiana katika kufanya mambo mbali mbali ya kijamii, ikiwa ni pamoja na sikukuu ya kuadhimisha miaka 77 ya Yanga, sikukuu za pasaka, kuchangia jamii na waliokumbwa na maafa, na kongamano la vijana lililolenga kuwaamsha vijana kuitambua nafasi yao katika Yanga ikiwa ni pamoja na kupata azimio la kuanzisha SACCOSS ya Yanga, ambapo maombi yapo kwa msajili Manispaa ya Ilala.

Haya yote nayataja ikiwa ni kuwashukuru kwa ushirikiano na ikiwezekana muweze kuyakamilisha yaliyobaki ambayo mtaona yalikuwa mazuri.Lakini pia tulipopata matatizo tulikuwa pamoja. Nichelee kusema tu kwamba tulisimama pamoja baada ya kujiuzulu Makamu Mwenyekiti wetu Ndugu Davis Mosha na mjumbe wetu ndugu Seif A. Seif, Ali Mayayi, na wengineo, kwani tulifungwa na katiba.

Tulisimama pamoja pia katika suala la kujiuzulu ndugu Yusuf M. Manji, aliyekuwa mdhamini mteule na mfadhili mkuu ambaye sasa ameonyesha nia ya kurudi nanyi mkaridhia mkutane naye.

Awali, tulitumia kila jitihada za kumrejesha lakini ikashindikana.Hata hivyo doa limetupata baada ya kufungwa na watani wetu goli 5 bila, ambapo kuna wanachama wanaoelewa na wasioelewa kabisa.Ninachokiona mimi ni usaliti wa hali ya juu uliombatana na matukio mbalimbali yaliyopita na yanayoendelea hadi kujaribu kupindua uongozi wa halali wa kidemokrasia. SIWATUHUMU WACHEZAJI MOJA KWA MOJA, isipokuwa mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo ule na sasa, inaonyesha kwamba kulikuwa na usaliti mkubwa ambao sisi hatukuweza kuubaini mapema.

Sioni mantiki katika hoja kwamba wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho n.k. Au ati mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo tuvune bao 5!Kwa wanaoijua Yanga, imewahi kuwa na madeni makubwa katika Hoteli mbali mbali, mawakala wa ndege n.k, na baadhi tumeyakuta na sisi tumekuja tukayalipa.

Hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwepo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki, na bado wachezaji walicheza kwa morali.Hata hivyo, utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatula kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuuondoa uongozi wa kidemokrasia.

Baada ya mapinduzi kushindikana na TFF kuonya kuhusu mapinduzi hayo, wazee kupitia msemaji wao , Mzee Akilimali wamesikika katika kipindi cha Michezo cha Redio moja maarufu hapa nchini wakidai kwamba ni bora Yanga ishushwe daraja au kufungiwa kuliko mimi kuendelea kuongoza!Hii imenikumbusha HEKMA ZA MFALME SELEMANI akiamulia ugomvi wa wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto naye akaamuru wamgawane nusu kwa nusu. Yule mwenye mtoto kweli alimuomba Mfalme amuachie mwenzie kuliko kumkata nusu.Kwa hekma hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika Uenyekiti wa Yanga kwani ni klab ninayoipenda hata kama sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.

Vile vile siko tayari kuona klab yangu ikisalitiwa au kuhujumiwa eti kwa sababu tu mimi ni kiongozi.Natumaini kamati ya utendaji kwa pamoja na wale tuliowateua chini ya ibara ya 29(3) ya katiba ya Yanga pamoja na bodi ya wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka kufikia mkutano mkuu kwa mafanikio zaidi. Nitaendelea kuwa mwanachama mwadilifu na nitatoa mchango wangu wa hali na mali pale nitakapo hitajika na nikiwa na uwezo wa kufanya hivyo.YANGA DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.Wasalaam,LLOYD NCHUNGA BIHARAGU.

Nakala kwa:-

Mama Fatma Karume,Mdhamini

Francis Kifukwe, Mdhamini

Bwana Yusuf Manji – Kwa taarifa

Thursday, May 24, 2012

MAMBO YA DAR LIVE



NCHUNGA KIBOKO, ATEUA WAJUMBE WAPYA KAMATI YA UTENDAJI

WAKATI wazee wa klabu ya Yanga wakimshinikiza Mwenyekiti wao, Lloyd Nchunga ajiuzulu, kiongozi huyo amezidi kuwa king’ang’anizi baada ya kutangaza kuteua wajumbe wawili wapya wa kamati ya utendaji.
Akizungumza kwa njia ya simu mjini Dar es Salaam jana, Nchunga aliwataja wajumbe hao wapya kuwa ni Dk. Maneno Tamba na Thobias Lingarangara.
Nchunga alisema uteuzi huo ulianza rasmi juzi na kuongeza kuwa, wajumbe hao wanachukua nafasi ya Ally Mayay na marehemu Theonest Rutashoborwa.
Kuteuliwa kwa wajumbe hao kunaifanya kamati hiyo sasa iwe na wajumbe sita. Wengine ni Salum Rupia, Tito Osoro, Sarah Ramadhani na Mbaraka Igangula, ambaye hata hivyo kuna taarifa kuwa alitangaza kujiuzulu juzi.
Nchunga alisema ameamua kuwateua wajumbe hao kutokana na mamlaka aliyonayo kikatiba na kwamba lengo ni kuifanya kamati ya utendaji iwe hai zaidi.
Wajumbe wa kamati hiyo waliojiuzulu hadi sasa ni Seif Ahmed, Mohamed Bhinda, Mzee Yusuph na Pascal Kihanga. Mwingine ni makamu mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo, Davis Mosha. “Nimewateua wajumbe hao wawili kutokana na mamlaka niliyonayo kikatiba kupitia kifungu cha 29 ibara ya (3) ya katiba ya Yanga,”alisema.
Kwa mujibu wa Nchunga, kifungu hicho kinaeleza kuwa, uongozi wa Yanga unaweza kujaza nafasi za wajumbe wa kamati ya utendaji waliojiuzulu ama kufariki dunia.
Alipoulizwa kuhusu msimamo wake, kufuatia shinikizo la kumtaka ajiuzulu kutokana na tuhuma mbalimbali, Nchunga alisema bado yeye ni kiongozi halali wa Yanga.
Alikanusha taarifa zilizozaa mjini Dar es Salaam jana kwamba, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa wajumbe wa kamati ya utendaji na angetangaza rasmi uamuzi wake huo kwa waandishi wa habari kesho.
"Sina mawazo wala mpango huo. Hao wanaosema hivyo wana ajenda zao, mimi naendelea kuitumikia klabu yangu, nashirikiana vyema na viongozi wenzangu kuanza kazi ya kusajili wachezaji wapya kimya kimya,"alisema Nchunga.

Coastal Union yamnasa Jerry Santo

KLABU ya Coastal Union ya Tanga ipo katika hatua za mwisho za kumsajili kiungo wa kimataifa wa Kenya, Jerry Santo, ambaye pia aliwahi kuichezea Simba.
Ofisa Habari wa Coastal Union, Edo Kumwembe alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, mazungumzo bado yanaendelea kati ya pande hizo mbili.
“Tupo kwenye usajili sasa na tayari tumeishawanasa wachezaji wawili na sasa tupo katika hatua ya mwisho ya kumsajili Jerry Santo,” alisema Edo. Uamuzi wa Coastal Union kumsajili Santo umekuja siku chache baada ya benchi la ufundi la timu hiyo kuamua kuwatema wachezaji tisa walioichezea katika ligi kuu ya Tanzania Bara msimu huu.
Miongoni mwa wachezaji hao ni Ally Ahmed ‘Shiboli’, Benard Mwalala,Ramadhani Wasso, Enock John, Laurent Mugia, Bakari Mohamed, Daudi Changula na Francis Busungu.
Katibu Mkuu wa Coastal Union, El- Siag alisema kwa njia ya simu kutoka Tanga kuwa, miongoni mwa sababu za kuwaacha wachezaji hao ni kushuka kwa viwango vyao.
El-Siag alisema ana matumaini makubwa kwamba, timu hiyo itafanya vizuri zaidi katika msimu ujao wa ligi na kushika nafasi za juu. Katika ligi ya msimu huu, Coastal Union ilishika nafasi ya tano.
Aliwataja wachezaji, ambao tayari wameshawasajili kwa ajili ya msimu ujao kuwa ni Nsa Job kutoka Villa Squad na kiungo Sudy Mohmed wa Toto Africans ya Mwanza.

Azam kucheza Kombe la Kagame

WASHINDI wa pili katika michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara, Azam wamepata nafasi ya kushiriki katika michuano ya Kombe la Kagame mwaka huu.
Kuingizwa kwa Azam katika michuano hiyo, kutaifanya Tanzania Bara iwakilishwe na timu tatu. Zingine ni mabingwa watetezi Yanga na mabingwa wa ligi kuu, Simba.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, maandalizi ya michuano hiyo yanakwenda vizuri.
Angetile alisema kwa vile Yanga itashiriki michuano hiyo kama mabingwa watetezi, Tanzania Bara imepewa nafasi zingine mbili kutokana na kuwa mwenyeji.
Kwa mujibu wa Angetile, tayari wadhamini wa michuano hiyo wameshapatikana na wanatarajiwa kutangazwa hivi karibuni katika mkutano wa viongozi wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Hii ni mara ya pili mfululizo kwa mashindano hayo kuchezwa Dar es Salaam. Katika mashindano ya mwaka jana, Yanga ilitwaa ubingwa baada ya kuichapa Simba bao 1-0 katika mechi ya fainali.
Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye alikaririwa wiki iliyopita akisema kuwa, baraza lake linafurahia mashindano hayo kuchezwa Dar es Salaam kutokana na wingi wa mashabiki na mapato makubwa.
Musonye alisema mashindano hayo na ya le ya Kombe la Chalenji yalikuwa na mafanikio makubwa kutokana na kuhudhuriwa na mashabiki wengi, ikilinganishwa na yanapofanyika katika nchi zingine zinazounda CECAFA.
Mwaka jana mashindano hayo yalitakiwa kufanyika Zanzibar, lakini kwa sababu ya uukosefu wa fedha, yalihamishiwa Sudan, ambayo nayo ilishindwa kuyaandaa kutokana na matatizo ya kisiasa.
Kwa mujibu wa Musonye, mapato ya viingilio yaliyopatikana katika mechi za mashindano hayo mwaka jana yalikuwa sh. bilioni 1.2 (dola 763,358 za Marekani).
Musonye alisema maandalizi kwa ajili ya mashindano ya mwaka huu yapo kwenye hatua za mwisho na yanatarajiwa kugharimu dola 600,000 (sh. milioni 944).
Mashindano ya mwaka jana yalidhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Castle. TBL ilidhamini mashindano hayo kwa sh. milioni 300.

SIMBA IANDAE MECHI MAALUMU YA KUMUENZI MAFISANGO

MWILI wa kiungo wa kimataifa wa Rwanda na klabu ya Simba, Patrick Mafisango ulizikwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye makaburi ya Kinkole yaliyopo nje kidogo ya Jiji la Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Mafisango alifariki dunia kwa ajali ya gari, usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita katika maeneo ya Chuo cha Ufundi (VETA), Chang'ombe, Dar es Salaam, akiwa anatoka matembezini katika klabu ya Maisha. Gari lake liliacha njia na kutumbukia mtaroni wakati akimkwepa dereva wa pikipiki.
Kifo cha Mafisango kimeacha simanzi kubwa kwa wanachama, viongozi na mashabiki wa Simba. Pia kimeacha simanzi kubwa kwa mashabiki wa soka wa Rwanda, ambako alikuwa ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo, Amavubi Stars.
Mafisango ni mzaliwa wa DRC, lakini alichukua uraia wa Rwanda kwa sababu ya soka. Hakuwahi kucheza soka na kupata umaarufu alipokuwa DRC. Alivipata vyote hivyo baada ya kwenda Rwanda kucheza soka ya kulipwa.
Mwanasoka huyo kipenzi cha wana-Msimbazi alifariki dunia katika kipindi, ambacho klabu yake ilikuwa ikimuhitaji zaidi kwa ajili ya michuano ya ligi na mechi za kimataifa. Alikuwa kipenzi cha wachezaji wenzake, viongozi na hata mashabiki wa Simba.
Ni kweli kwamba Mafisango alikuwa na matatizo yake binafsi na ndio sababu uongozi wa Simba uliwahi kumsimamisha, lakini kutokana na umuhimu wake kwenye kikosi cha timu hiyo, alisamehewa na kuendelea kupiga mzigo.
Kwa wanaofuatilia soka ya Tanzania kwa makini, bila shaka watakubaliana na safu hii kwamba, Mafisango alikuwa na vituko nje ya uwanja, lakini alipokuwa uwanjani, ilikuwa habari nyingine.
Mafisango aliingia nchini miaka mitatu iliyopita na kusajiliwa na Azam. Lakini baada ya viongozi wa klabu hiyo kuonekana kukerwa na vituko vyake, waliamua kumuuza kwa klabu ya Simba kwa kubadilishana na kiungo, Abdulrahim Humud.
Ni kuanzia hapo Mafisango akaanza kujipatia umaarufu mkubwa kutokana na kuimudu vyema nafasi yake ya kiungo mkabaji ama kiungo mshambuliaji. Alikuwa mchezaji wa aina ya pekee, ndio sababu alikuwa kipenzi cha mashabiki wa Simba.
Kutokana na kuguswa na kifo chake, viongozi wa Simba, akiwemo Mwenyekiti, Ismail Aden Rage walipatwa na kigugumizi wakati wa kuuaga mwili wake. Wachezaji wenzake walishindwa kujizuia kulia, hasa kipa Juma Kaseja na mshambuliaji Haruna Moshi 'Boban', ambaye alikuwa swahiba mkubwa wa Mcongoman huyo.
Ni wazi kuwa Simba imepoteza mchezaji mzuri na muhimu kwenye kikosi chake na itachukua muda mrefu kumpata mchezaji mwingine wa kuweza kuziba pengo lake.
Kinachosikitisha ni kwamba, viongozi wa Simba hawakumtendea haki Mafisango. Walifanya vizuri kuandaa utaratibu wa kuuaga mwili wake na pia kuusafirisha kwenda DRC kwa mazishi, lakini hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyekuwepo kwenye msafara huo.
Kwa mtazamo wangu, mwili wa Mafisango ulipaswa kusindikizwa na aidha Rage ama makamu wake, Godfrey Nyange. Lakini ajabu ni kwamba, uongozi uliamua kumteua Mzee Kinesi kusindikiza mwili huo, akiwa amefuatana na Boban.
Hili ni kosa kubwa. Uongozi wa Simba ulipaswa kumpa heshima mchezaji huyo kwa kiongozi wake mmoja wa ngazi ya juu kuusindikiza mwili wake na kuukabidhi kwa wazazi wake. Sielewi ni hofu gani waliyokuwa nayo viongoziSimba hata wakashindwa kufanya hivyo. Ni pia sielewi ni dharura ipi iliyowafanya wasiende DRC kumsindikiza mchezaji wao kipenzi.
Waswahili wana msemo usemao, thamani ya mtu huonekana pale tu anapokuwa hai duniani. Akishafariki basi na thamani yake nayo inakuwa imekwisha.
Nawapongeza sana Simba kwa kuandaa utaratibu mzuri wa kuuaga mwili wa Mafisango, lakini sikubaliani na kisingizio chochote kitakachotolewa kwa nini mmoja wao alishindwa kuusindikiza mwili wa mchezaji huyo kwao. Nawapongeza pia viongozi wa Simba kwa uamuzi wao wa kutotumia tena jezi namba 30 iliyokuwa ikivaliwa na Mafisango kwa lengo la kumuenzi mchezaji huyo, lakini nadhani bado kuna kitu kingine kinachopaswa kufanywa ili kuienzi familia yake.
Kwa mtazamo wangu, nadhani ni vyema viongozi wa Simba waandae mechi maalumu ya kimataifa ya soka ili kuchangisha fedha kwa ajili ya kuisaidia familia yake, hasa watoto wake watatu, ambao bado wadogo na bila shaka wanahitajika kusoma.
Nina hakika hiyo itakuwa njia nyingine nzuri zaidi ya kumuenzi Mafisango na kuwafanya wazazi na ndugu zake waiheshimu Simba na Tanzania kwa jumla. Mechi hiyo pia itawafanya wazazi na ndugu wa Mafisango waone mtoto wao hakupotea njia kuja kucheza soka Tanzania.
Njia nyingine nzuri ya kumuenzi Mafisango ni kwa wachezaji wa timu hiyo kucheza kwa kujituma kama alivyokuwa akifanya kiungo huyo, ambaye kila alipofanya kosa uwanjani lililoigharimu timu yake, alifanya kila njia kujirekebisha na kuwapa furaha mashabiki wa timu hiyo.

Uche Jombo avunja ukimya

LAGOS, Nigeria
HATIMAYE mcheza filamu wa kike mwenye mvuto nchini Nigeria, Uche Jombo amethibitisha kufunga ndoa hivi karibuni nchini Venezuela.
Uche ameamua kuvunja ukimya huo baada ya vyombo kadhaa vya habari nchini Nigeria kuripoti wiki iliyopita kwamba, amefunga ndoa kwa siri.
Mwanadada huyo aliripotiwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa Kimarekani.
“Ndio ni kweli, lakini siwezi kutoa taarifa zingine zaidi kwa sasa. Lakini naahidi kufanya hivyo hivi karibuni,”alisema Uche.
Kwa mujibu wa Uche, walifunga ndoa hiyo Mei 16 mwaka huu katika mji wa Puerto Rico na kuhudhuriwa na watu kadhaa maarufu, akiwepo rafiki yake wa karibu, Desmond Elliot.

D'Banj, Kanye West wacheza filamu ya ujambazi Qatar


LAGOS, Nigeria
MWANAMUZIKI nyota wa miondoko ya hip hop wa Nigeria, Dapo Oyebanji a.k.a D’Banj na mwanamuziki mwenzake wa miondoko hiyo wa Marekani, Kanye West wameshiriki kucheza filamu mpya.
Hata hivyo, filamu hiyo bado haijapewa jina, lakini inatarajiwa kuingia sokoni hivi karibuni.
Picha za filamu hiyo, inayoelezewa kuwa ni ya aina yake, zimepigwa nchini Qatar na wanamuziki hao wamecheza nafasi ya ujambazi.
D’Banj wamekuwa wakitawala vyombo vya habari nchini Nigeria na Marekani kutokana na matukio mbalimbali. D’Banj hivi karibuni alitengana na bosi wake, Don Jazzy wakati Kanye ameripotiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kim Kardashin.

Nimepata mpenzi wa kweli-Funke Akindele



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Funke Akindele amesema anamshukuru Mungu kwamba kwa sasa amempata mpenzi wa kweli na anayempenda kwa dhati.
Akindele ameueleza mtandao wa naijerules wiki hii kuwa, kwa sasa yupo kwenye mapenzi mazito na haoni tatizo kukiri ukweli huo.
“Mimi si mtoto mdogo na naelewa nini maana ya kuwa katika mapenzi. Hili ni penzi la kweli. Nimempata nimpendaye,”alisema mcheza filamu huyo machachari wa Nollywood.
Alipoulizwa jina la mpenzi wake huyo, Akindele hakuwa tayari kulitaja. “Kuwa na furaha kwa ajili yangu, nimempata mpenzi wa kweli,”alisema.

Siamini ushirikina katika muziki-Jose

MWANAMUZIKI Jose Mara wa bendi ya muziki wa dansi ya Mapacha Watatu amesema, haamini iwapo ushirikina unaweza kuisaidia bendi kupata mafanikio.
Jose amesema mashabiki wanaweza kuvutiwa na nyimbo za bendi iwapo zimepigwa kwa mpangilio mzuri na mashairi yake yanatoa ujumbe muhimu kwa jamii.
Mwimbaji huyo wa zamani wa bendi ya FM Academia alisema hayo wiki hii mjini Dar es Salaam alipokuwa akijibu swali aliloulizwa iwapo ni kweli mauzo ya albamu za muziki hutegemea zaidi ndumba.
Alisema hana hakika iwapo viongozi wa FM Academia walitumia ndumba kuongeza mauzo ya albamu yao ya kwanza, ambayo ilifanya vizuri zaidi sokoni kuliko zilizofuatia.
“Sikuwahi kuwa kiongozi FM Academia, hivyo kama jambo hilo lilifanyika, liliwahusu wao, mimi sikushiriki kabisa, ndio kwanza nasikia kutoka kwako,”alisema mwimbaji huyo mwenye sauti yenye mvuto.
“Lakini binafsi naamini kuwa, ukiimba kitu kizuri, lazima mashabiki watakikubali, lakini siamini kabisa mambo ya ushirikina,”aliongeza.
Jose pia alikanusha madai kuwa, mmiliki wa bendi ya Twanga Pepeta International, Asha Baraka amekuwa na bifu na bendi ya Mapacha Watatu.
Alisema kama kweli kuna bifu kati yao, bifu hilo ni la kibiashara zaidi kwa sababu Asha hawezi kuchukia kutokana na wanamuziki wake kuhama na kujiunga na bendi zingine.
Hata hivyo, Jose alisema wakati mwingine, bifu kati ya bendi za muziki zimekuwa zikianzishwa na kukuzwa na vyombo vya habari bila ya wanamuziki kufahamu lolote.
Bendi ya Mapacha Watatu inamilikiwa na Jose, aliyetokea FM Academia na Kalala Junior na Khalid Chokoraa waliotokea Twanga Pepeta.
Jose alisema wasanii wanatakiwa kuwa waangalifu katika kazi zao kwa sababu wanapaswa kuwa na maisha yao wenyewe, hivyo wanapopata mwanya ama malisho mazuri, hawatakiwi kulaza damu.
“Waswahili wanasema, ujinga wa ujanani ni umaskini wa uzeeni,”alisema Jose.
Kwa sasa, Jose ameamua kuacha kabisa kunywa pombe. Alifikia uamuzi huo tangu mwaka jana kwa lengo la kutunza sauti na afya yake.
Alikiri kuwa, wimbo wake wa Buriani Mama ni tukio la kweli. Alisema aliimba wimbo huo kwa lengo la kumuenzi marehemu mama yake na kwanza hata kaburi lililotumika kwenye video ya wimbo huo ni la mama yake.

NYAMWELA: Sina mpango wa kurudi tena Twanga Pepeta

MCHEZA shoo maarufu nchini, Hassan Mussa ‘Super Nyamwela’ amesema hana mpango wa kurejea katika bendi yake ya zamani ya Twanga Pepeta International.
Nyamwela amesema muziki kwa sasa ni kama mchezo wa soka hivyo msanii ama mwanamuziki anapaswa kufanyakazi kimkataba na kwa kuzingatia maslahi bora zaidi.
Dansa huyo machachari alisema hayo mwanzoni mwa wiki hii alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Mkasi kilichorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Channel Ten.
“Kusema ule ukweli, siwezi kurudi Twanga Pepeta, nipo Extra Bongo kimkataba,”alisema dansa huyo, ambaye pia ni mahiri kwa ubunifu wa minenguo mbalimbali.
“Muziki kwa sasa ni sawa na mchezo wa soka. Msimu ukiisha, unatafuta timu nyingine na kuingia nayo mkataba,”aliongeza msanii huyo.
Alisema kinachofanyika kwa sasa ni maelewano kati ya msanii na viongozi wa bendi na kwamba kinachozingatiwa ni maslahi kati ya pande zote mbili.
Dansa huyo alisema kubadili maisha ni jambo zuri kwa mtu yeyote na kuongeza kuwa, jambo la msingi la kuzingatia ni kutazama kipi bora kati ya umaarufu na kuwa na maisha mazuri.
Nyamwela alisema yeye ni tofauti na wacheza shoo wengi wa Bongo kwa sababu mbali ya kucheza stejini, anaimba, kurapu na kutunga nyimbo.
“Hadi sasa nimesharekodi albamu mbili na zipo sokoni. Hivyo usimuone mcheza shoo ukamdharau kwamba hana lolote. Wengine tunafanyakazi hii kwa malengo,”alisema.
Dansa huyo ametamba kuwa, anazo kila sababu za kujivunia kuwapika wacheza shoo wengi wa Bongo. Alisema katika wacheza shoo 100 wa Kibongo, asilimia 99 wamepitia kwake.
Nyamwela anao watoto wawili aliozaa na mkewe wa kwanza, Halima White, ambaye kwa sasa ni marehemu. Alisema kwa sasa, anajiandaa kuoa mke wa pili.
Msanii huyo alianza kujihusisha na muziki wa dansi mwaka 1990 kabla ya kuanzisha kundi lake lililokuwa likijulikana kwa jina la Billbums, ambalo lilikuwa likifanya maonyesho yake katika ukumbi wa Club Billicanas, Dar es Salaam.
Kundi hilo lilifanyakazi kwenye ukumbi huo kwa miaka mitano na lilikuwa na nguvu kuliko bendi za muziki wa dansi. Alisema akiwa katika kundi hilo, aliweza kujifunza vitu vingi kuhusu muziki, vikiwemo vya kimataifa.

FLAVIANA MATATA AKUMBUKA MBALI

Mwanamitindo maarufu wa Tanzania, Flaviana Matata akibubujikwa na machozi wakati wa ibada ya kuwakumbuka watu waliofariki katika ajali ya meli ya MV Bukoba iliyotokea miaka 16 iliyopita kwenye Ziwa Victoria. Ibada hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye makaburi ya Igoma mjini Mwanza. Mrembo huyo, ambaye alimpoteza mama yake kutokana na ajali hiyo, alitoa misaada ya vifaa mbalimbali vya kujikinga na ajali.

Kikosi cha Z'bar Kombe la Dunia chatajwa

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, Hemed Suleiman 'Moroko' ametangaza kikosi cha wachezaji 18 kitakachoshiriki katika mashindano maalumu ya Kombe la Dunia kwa nchi zisizo wanachama wa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), 'Viva World Cup'.
Mashindano hayo yamepangwa kuanza kutimua vumbi Juni 4 mwaka huu nchini Kurdistan, kaskazini mwa Iraq na yatazishirikisha timu za mataifa tisa.
Ofisa Habari wa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA), Munir Zakaria aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa juzi kuwa, kikosi hicho kimeshaanza kambi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano hayo.
Aliwataja wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho, timu wanazotoka zikiwa kwenye mabano kuwa ni Ismail Khamis (Mafunzo), Awadh Juma (Mtibwa Sugar), Khamis Mcha (Azam FC), Juma Othman Mmanga (Jamhuri), Mohammed Abdulrahim (Mafunzo), Abdulhalim Humud na Abdughan Gulam (wote Azam FC).
Wengine ni Abbas Nassor (Miembeni United), Ali Badru (Al Canal, Misri), Amir Hamad (JKT Oljoro), Abdi Kassim 'Babi' (Azam FC), Suleiman Kassim (African Lyon), Nadir Haroub (Yanga SC), Ali Mohammed (Super Falcon), Yussuf Makame (Mafunzo), Salum Shebe (Al Mudheiby, Oman), Sabri Ramadhan (Omani Club) na Gharib Mussa (African Lyon).
Zakaria alisema wachezaji wanne wanaocheza ligi kuu Tanzania Bara hawakuitwa kutokana na kuwemo kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars, kinachojiandaa kwa mechi ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014 dhidi ya Ivory Coast.
Aliwataja nyota hao kuwa ni Nassor Masoud 'Cholo' (Simba SC), Aggrey Morris, Waziri Salum na Mwadini Ali wanaokipiga na Azam FC.
Kwa mujibu wa Zakaria, kikosi hicho cha Zanzibar Heroes kitakuwa kikifanya mazoezi kwenye uwanja wa Mao Dzedong na kitakuwa chini ya Moroko akisaidiwa na Hafidh Muhidin.
Wakati huo huo, Zakaria amesema Zanzibar Heroes inatarajiwa kucheza mechi moja ya kirafiki ya kujipima nguvu dhidi ya Malawi.
Ofisa huyo wa ZFA alisema mechi hiyo inatarajiwa kupigwa Mei 28 mwaka huu kuanzia saa 2.30 usiku kwenye Uwanja wa Amaan.
Alisema timu hiyo inatarajiwa kuwasili Zanzibar asubuhi ya siku hiyo kwa boti ikitokea Dar es Salaam, ambako itacheza mechi yake ya kwanza ya kirafiki keshokutwa dhidi ya Taifa Stars.
Zakaria alisema Zanzibar Heroes inatarajiwa kuondoka nchini Juni 2 mwaka huu kwenda Iraq kwa ajili ya kushiriki katika mashindano hayo.
Alisema timu hiyo itaagwa Juni Mosi mwaka huu kwa kukabidhiwa bendera ya taifa na itaondoka Zanzibar kwa ndege ya Precision Air kabla ya kuunganisha ndege ya Qatar Airways.