KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Msechu arekodi na Kidumu


BAADA ya kung’ara katika shindano la mwaka huu la Tusker All Stars, msanii machachari wa muziki wa kizazi kipya nchini, Peter Msechu ameibuka na kibao kisemacho Relax.
Msechu amerekodi kibao hicho kwa kushirikiana na msanii machachari kutoka nchini Rwanda, Kidumu.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Msechu alisema amefurahi sana kupata nafasi ya kurekodi na Kidumu kwa vile ni ndoto aliyokuwa nayo kwa miaka mingi.
Msechu alisema alikuwa na ndoto ya kurekodi na Kidumu kwa miaka mingi, lakini hakuweza kufanikiwa kwa vile alikuwa bado msanii mchanga.
Alisema katika maisha yake kiusanii, amepitia misukosuko mingi, ikiwa ni pamoja na kutembea kwa miguu umbali mrefu kuwatafuta wasanii maarufu ili wamsaidie katika kurekodi nyimbo zake.
“Ninachoweza kusema ni kwamba, hatimaye zile ndoto nilizokuwa nazo kwa miaka mingi, sasa zimeanza kutimia,”alisema.
Mbali na kurekodi na Kidumu, Msechu pia amepata nafasi ya kurekodi wimbo wake wa Unaniumiza kwa kushirikiana na kiongozi wa Akudo Impact, Christian Bella.
Vibao vingine vilivyomjengea umaarufu mkubwa Msechu ni pamoja na Hasira hasara na Poleni.
00000

No comments:

Post a Comment