KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Mwaikimba amwaga wino Azam FC


MSHAMBULIAJI Gaudence Mwaikimba wa Moro United amejiunga rasmi na Azam FC kwa ajili ya mzunguko wa pili wa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.
Ofisa Habari wa Azam, Jafari Iddi alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, tayari mshambuliaji huyo ameshatia saini mkataba wa kuichezea timu hiyo.
Jafari alisema wameamua kumsajili Mwaikimba kwa lengo la kuziba pengo la mshambuliaji wao kutoka Ghana, ambaye ameachwa kutokana na kiwango chake kushuka.
Msemaji huyo wa Azam alisema, Mwaikimba anatarajiwa kuanza mazoezi na timu hiyo mara baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Chalenji.
Alisema wanaamini, Mwaikimba atashirikiana vyema na mshambuliaji John Bocco na Mrisho Ngassa kuunda safi kali ya ushambuliaji.
Kwa mujibu wa Jafari, lengo la timu yake ni kuhakikisha kuwa, wanamaliza msimu huu wa ligi wakiwa mabingwa ama kushika nafasi ya pili ili waweze kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.
Kwa sasa, Mwaikimba yumo kwenye kikosi cha Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji, inayotarajiwa kuanza kesho mjini Dar es Salaam.
Mwaikimba alianza kujipatia umaarufu alipokuwa akichezea Ashanti kabla ya kuchukuliwa na Yanga na baadaye kuhamia Kagera Sugar ya Bukoba.
Mchezaji huyo alikuwemo kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars kilipokuwa chini ya Kocha Marcio Maximo kutoka Brazil kabla ya kutemwa kwa madai ya kiwango chake kushuka.

No comments:

Post a Comment